Ijumaa, 7 Oktoba 2016

Makosa Manne (04) Ambayo Watu Wamekuwa Wakiyarudia Rudia Na Kuwagharimu Kwenye Maisha Yao.


Kwenye maisha tunayoishi kuna mambo mbali mbali tunakutana nayo. Tunakumbana na matatizo ya maisha, tunapata changamoto za maisha. Vile vile tunapata mafanikio ya maisha. Watu tunakuwa na furaha tunapopata mafanikio. Lakini tukija upande wa pili huwa tunapatwa na huzuni tunapoyakosa mafanikio. Kwenye maisha ya kila siku kuna makosa mbali mbali ambayo watu wanakuwa wanayarudia. Makosa hayo yanapelekea kugharimu mafanikio yao kwenye maisha.

Haya hapa ni makosa 4 ambayo watu wanayafanya:
1.           Kufanya Vitu Ambavyo huvipendi
Hakuna kosa baya kwenye maisha tunayoyaishi kama kufanya mambo ambayo huyapendi. Tumeona watu wengi wamezoeya kufanya kazi wasizozipenda. Wanafunzi wanasoma kozi ambazo hawazipendi, na watu wanafanya mahusiano na watu wasiowapenda. Matokeo yake ni kupata matatizo ambayo yanakuwa ni gharama kwenye maisha. Unapoamua kuachana na vitu usivyovipenda utajikuta unatumia muda wako vizuri. Unatumia nguvu zako nyingi kwenye shughuli zenye maana kwako na maisha yako.
2.           Kuishi Kwa Kufikiria Mambo Yaliyopita
Tunapoteza muda wetu mwingi kwa kufikiria makosa tuliyoyafanya nyuma. Mambo yaliyopita yamepita hatuna ujanja wa kuyarudisha tena. Kuendelea kufikiria makosa ambayo umeshayafanya nyuma kunaweza kukusababishia kurudi nyuma kwenye maisha. Epukana na mawazo ya nyuma badala yake weka juhudi kwenye kile unachokifanya kwa sasa.
3.           Hatuziendei  Ndoto Zetu
Hili ni kosa jengine tunalolifanya kila siku kwenye maisha yetu. Watu wengi wanakuwa na mambo mengi yasiyo ya msingi kwenye vichwa vyao. Watu wanakuwa na tabia ya kutaka kufanya kila kitu kinachokuja mbele yake. Matokeo yake wanashindwa njiani kwa sababu amefanya kitu ambacho hakihusiani na ndoto yake.
4.           Hatuna Mipango
Maisha tunayoishi yanahitaji malengo na mipango. Tunahitaji kupanga maisha yetu ya kila siku, wiki, mwezi na hata mwaka. Maisha bila mipango ni kosa kubwa linalopelekea kufeli kwenye maisha yetu. Kama hatupendi kufanya kosa hili basi njia mzuri ya kufanya ni kuandika mipango yetu. Mipango inayoelezea  kila hatua tunayotaka kuifikia.
Epuka makosa haya ambayo watu wengi wamekuwa wakiyarudia rudia kila siku. Na kosa kubwa ambalo huwa tunalifanya ni lile la kurudia rudia makosa ambayo tunaendelea kuyafanya. Waswahili wanasema kufanya kosa sio kosa kosa ni kurudia kosa. Hivyo ushauri wangu kwenye makala hii ni kukusihi usirudie makosa.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA