Unapoingia kwenye biashara
unatakiwa uwe makini ili kuweza kutengeneza faida ya biashara. Wafanyabiashara
wengi wamekosa uwezo wa kuongoza biashara zao ili ziweze kuwapatia mafanikio.
Na hii inatokana na makosa wanayoyafanya kila siku kwenye biashara zao.
Yafuatayo ni makosa 9
ambayo wamiliki wa biashara wanayafanya kwenye biashara zao:
1.
Kukosa Lengo Linaloeleweka
Mfanyabiashara lazima awe na
muda wa kutosha wa kutengeneza dira na mtazamo wa biashara anayoifanya. Ni
muhimu kufanya hivyo kwenye biashara yoyote ile unayotaka kuifanya. Biashara
inahitaji maelezo yanayoelezea kwa nini inatakiwa kuwepo. Biashara ambayo
imekosa malengo yanayoeleweka ni rahisi kufeli.
2.
Kukosa Mipango
Wafanyabiashara wengi wanakosa
mipango mizuri katika kuendesha biashara zao. Biashara lazima iwe na mipango.
Haijalishi kama ni biashara ndogo au kubwa. Ukishindwa kupanga kwenye biashara
unayoifanya basi unakaribisha kushindwa.
3.
Kukosa Bajeti
Huwezi kuendesha biashara pasipo
kuwa na bajeti ya biashara. Ili kuweza kuona faida ya biashara ni muhimu
kuandaa bajeti ya mwaka. Hii itakusaidia kufuatilia mipango na malengo ya
biashara. Biashara nyingi zinakufa kila siku kwa sababu zinaendeshwa bila ya
bajeti.
4.
Kukosa Wafanyakazi Wanaoweza
Kuwajibika
Biashara ambayo itakosa
wafanyakazi ambao sio wawajibikaji kwenye kazi zao ni vigumu biashara
kuendelea. Biashara ambayo inalipa mishahara lakini haitimizi malengo yake
haiwezi kufanikiwa. Kuwaongoza wafanyakazi katika kufuatilia utendaji wao
kutakusaidia usifanye makosa yanayoweza kujirudia katika biashara.
5.
Huendani Na Mabadiliko Ya Soko
Kwenye biashara mabadiliko ya
soko hutokea mara kwa mara. Ni muhimu kuangalia soko linaendaje ili biashara
yako iendane na mabadiliko hayo. Soko linaweza kuhusisha na mabadiliko ya
teknolojia au mahitaji ya wateja.
6.
Huwafahamu Wateja
Ni muhimu kuwafahamu wateja wako
wanahitaji nini. Wateja ndio wanaoweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye
biashara yako. Biashara inaweza kuanguka au kusimama kutokana na wateja. Hivyo
jenga ukaribu na wateja . Kufanya hivyo kutakusaidia usifanye kosa hili la
kutowafahamu wateja ambao wanaweza kuangusha biashara yako.
7.
Humjali Mfanyakazi Wako
Mfanyakazi wako ndiye mteja wa
kwanza katika biashara yako. Mpatie mfanyakazi wako mafunzo ya kutosha
yanayoendana na biashara yako. Fuatilia kwa ukaribu maendeleo yake . Anapofanya
vizuri mpongeze kwa zawadi. Mfanyakazi anayeongozwa vizuri lazima awe na
furaha. Furaha yake ni matunda mazuri katika uzalishaji wa biashara.
8.
Kukosa Mawasiliano Mazuri
Mawasiliano mabaya ni sumu
kwenye biashara zilizo nyingi. Biashara yenye mafanikio inatengeneza mtandao
mzuri wa mawasiliano baina ya mteja na mfanyakazi.
9.
Huangalii Njia Za Kuboresha
Biashara yenye mafanikio
huangalia njia za uboreshaji wa huduma inazotoa. Mmiliki wa biashara ana wajibu
wa kuangalia njia za kuboresha huduma kwa wateja wake. Biashara ambayo haina
mpango wa uboreshaji huduma ni rahisi kufeli.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena