Kazi ngumu ya kukamilisha kila kitu ni kuanza. Katika maisha hakuna jambo gumu kama kuishawishi akili yako ili iweze kuanza. Lakini mara unapoanza unakuwa tayari umefungua milango ya kukamilisha. Kwenye kazi zetu na kwenye biashara tunakuwa na shauku kutekeleza malengo makubwa, lakini tunapokuja kwenye suala la utekelezaji tunakuwa tunasumbuliwa na jinamizi la kuanza.
Kama utaangalia watu walio wengi
walioweza kufanikiwa walikuwa na kila sababu ya mafanikio kutokana na kuweza
kugundua siri hii ya mafanikio.
Watu Waliofanikiwa Waliweza
Kuanza.
Ukiwa utachunguza tabia za watu
waliofanikiwa basi tunaweza kusema waliofanikiwa waliweza kuthubutu kuanza
kabla hawajawa tayari kuanza. Tambua kwamba hakuna siri nyengine. Hakuna kitu
maalumu ambacho watu waliofanikiwa wamezaliwa nacho lakini ambao wameshindwa
kufanikiwa hawana. Wao kwao ilikuwa ni kazi rahisi kuweza kuwa na msukumo wa
kuanza kufanya kitu kipya.
Kitu Kibaya Zaidi Ambacho
Kinaweza Kukutokea.
Moja ya hofu yetu kubwa ni
kuonekana kuwa tumeshindwa. Tumekuwa na hofu kufeli zaidi kuliko kuonekana
tunafeli. Ndio maana watu wengi kabla ya hata kusubiri kushindwa wanakuwa
tayari wamerudi nyuma na kushindwa kumalizia vitu walivyo vianza.
Lazima watu tutambue kwamba
katika maisha kuna kufaulu na kufeli, na daima mafanikio yanakuja baada ya
kufeli. Mfano kama umeamua kuanzisha biashara lakini ukaishia njiani kwa sababu
ya kupata hasara. Lakini mara nyengine ukaamua kuanzisha biashara utakuwa
tayari umepata uzoefu wa kutosha kuhakikisha kosa la kupoteza halijirudii tena.
Tambua kwamba mafanikio ni
muendelezo wa kufeli. Na huwezi kufeli bila ya kuanza. Unatakiwa ufeli mara
nyingi zaidi ndio uweze kujifunza mafanikio. Na ipo njia moja tu ya
kufeli moja kwa moja: Njia hiyo ni kushindwa kuanza.
Unapoamua kuanza ndio unakuwa
umeanza kupiga hatua mbele. Hata kama umeanza kidogo lakini huo ndio mwanzo
mzuri wa mafanikio . Usikubali kuendelea kuwa na hofu ya kuogopa kuanza.
Habari Njema Kwako.
Hofu kubwa ambayo inawarudisha
watu nyuma ni kutokana na kuwa hawako tayari na kuanza. Tuchukulie mfano
umeamua kuanzisha biashara ya kutengeneza pesa kwa njia ya mtandao kwa kutumia
blogi. Unapoanza biashara hii utaona unahitaji kujuwa kila kitu kuhusiana na
blogi. Hivyo utatumia muda wako bila ya kuupoteza kuweza kujifunza mambo mbali
mbali yanayohusiana na blogi. Wakati unaendelea kujifunza unakuwa na muda mzuri
wa kujiandaa kutengeneza blogi ya kitaalamu. Kumbuka mwanzo unaanza ulikuwa
unaona mambo ni magumu lakini unapokuwa kwenye mchezo kila kitu unakiona ni
rahisi kwako. Na njia nzuri ya kujua kila kitu ni kuendelea kujifunza na
kufanya kile ulichojifunza.
Hakuna siri nyengine ya
mafanikio zaidi ya kuanza.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena