Jumamosi, 5 Novemba 2016

Muhimu Kuzifahamu Tabia Hizi Nne (04) Za Pesa Kwa Kila Mfanyabiashara


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na tabia muhimu kwa kila mfanyabiashara kuzifahamu kwa ajili ya kuwa na usimamizi mzuri wa pesa.

Usimamizi wa pesa ni ujuzi muhimu kwa Mfanyabiashara yeyote anayetaka kufanikiwa katika maisha yake. Ni muhimu pia kuzingatia matumizi mazuri ya pesa ili uweze kukua kimaisha.

Mafanikio katika biashara yako yanategemea na ujuzi na ufuatiliaji wa tabia hizi za pesa kwa muda mrefu. Zijue tabia hizi za pesa zinazomfanya kila mfanyabiashara aweze kujiletea mafanikio makubwa katika biashara yake na maisha yake kwa ujumla.

Zifuatazo ni tabia za pesa unazotakiwa kuzikuza ili kufanya vizuri katika biashara yako:

1.           Kupitisha Mawazo Ya Akiba
Kuokoa fedha ni muhimu sana kwa maisha ya afya ya kifedha. Kuweka akiba kutakusaidia kuwa na matumizi mazuri ya pesa na hii utaweza kufanya matumizi yale ambayo ni ya lazima pekee. Utunzaji wa pesa utakuwezesha kufanya matumizi ambayo umeyafanyia bajeti tu. Na hii ndio inayowafanya wafanyabiashara kuweza kuwa na mtaji wa kutosha na kupelekea ukuaji mzuri  wa biashara anayoifanya.

Hatua muhimu ya kufuata ili uweze kuweka akiba  ni kujenga tabia ya kuhifadhi fedha kwanza kabla hujafanya matumizi ya aina yoyote. Na hii unaweza kuifanya kwa kutenga kiasi fulani cha pesa ambacho unaweza kukiweka kwenye akaunti maalumu ya biashara na kufanya matumizi kutokana na mahitaji ya bajeti yako.

2.           Tumia Fedha Kwa Uangalifu
Kanuni muhimu ya kuwa mfanyabiashara ni kwamba unakuwa mbahili katika pesa zako. Hakikisha pesa zako hazitumiki kwa mambo ambayo  hayaongezi faida kwenye biashara. Kutumia pesa kwa uangalifu kutakusaidia kujijengea nidhamu mzuri ya pesa. Matumizi mazuri ya pesa yatakusaidia kuokoa pesa nyingi na kupata mapato ya ziada.

Tabia hii ya kutumia kwa uangalifu kutazalisha matokeo chanya juu ya biashara yako na maisha yako kwa ujumla.

3.           Hesabu Kila Unachonunua
Kama mfanyabiashara ni wajibu wako kufanya hesabu kwa kila shilingi unayoifanyia matumizi. Kufanya hesabu kwa kila senti unayotumia kutafungua macho yako kwa matumizi yasiofaa. Hii itakusaidia kuweza kuzuiya tabia mbaya ya matumizi mabaya ya pesa zako.

4.           Yape Kipaumbele Matumizi Yako
Ili kupata fedha yako moja kwa moja, inakupasa kuanza kuendeleza tabia ya kuweka kipaumbele matumizi ya pesa zako. Kutengeneza tabia hii itakusaidia kuamua ni bidhaa gani inahitajika kwa wakati huo. Kuweka kipaumbele kwa mahitaji yako ya muhimu zaidi kunaweza kukusaidia kuwa meneja mzuri wa pesa zako. Njia bora ya kila mfanyabiashara mwenye mafanikio ni kuanza kutengeneza tabia nzuri ya kuwezesha ukuaji wa biashara yako. Kupanga fedha yako ni mwanzo mzuri kwa ukuaji wa biashara yako.

Kama mfanyabiashara unayetafuta mafanikio hakikisha unaendeleza tabia hizi. Hakiksha unaweka akiba, Unatumia fedha kwa uangalifu, Unafanya hesabu kwa kila unachonunua na tumia kwa kuwa kipaumbele.

 
Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
 

 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA