Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.
Leo hii napenda kuwashirikisha
wasomaji wetu makala inayohusiana na kanuni muhimu kwa ajili ya kupata
mafanikio makubwa kwenye maisha yako.
Kila mtu anapenda afanikiwe.
Mafanikio makubwa hayawezi kuja hivi hivi tu. Kama unataka kupata mafanikio
makubwa, ni lazima ufanje zaidi ya kawaida yako. Ni lazima uchukue hatua kubwa
zaidi. Lazima ndoto zako ziwe kubwa zaidi kuliko vile unavyotarajia.
Katika Makala hii nitakuelezea
kanuni hizi tano ambazo zitakuweka kwenye njia sahihi itakayokupeleka kufikia
mafanikio yako makubwa.
1.
Panga Malengo Yako Kwa Kiwango
Cha Juu Unachoweza Kukifikia
Kwanza ni muhimu kuamini kwamba
huwezi kufikia mafanikio makubwa pasipo na kuwa malengo uliyoyaweka wazi.
Malengo yako ni ule uwezo wako wa kuona sasa hivi pale ambapo unataka kuwa
katika maisha ya baadaye. Na hii ndio sababu muhimu ya wewe kuwa ni lazima uwe
na ndoto kubwa. Panga malengo ambayo yatakusukuma wewe na kukutoa nje ya ukanda
wa faraja yako ya kila siku. Lakini pia ni muhimu kuweka malengo ambayo unaweza
kuyafikia ile usiweze kuchoka njiani na kupata msongo wa mawazo. Kama utakuwa
umeelewa vizuri basi utakuwa tayari uko kwenye njia ya mafaniko.
2.
Chukua Hatua Ya Kufanya Mambo
Makubwa
Kama huwezi kuruka basi kimbia.
Kama huwezi kukimbia basi tembea. Kama huwezi kutembea basi tambaa. Lakini njia
yoyote utakayopitia iwe ni kusonga mbele. Tambua kwamba haitoshi kupanga
malengo pekee bali pia lazima uchukue maamuzi ya kufanya ili uweze kufanikiwa.
Unapoweka malengo yako ni muhimu kuweka mfumo wa kukusaidia kuhakikisha kwamba
malengo yako yote umeyapanga katika hatua na tarehe ya mwisho ya kuweza
kuyafikia. Na kufanya hivyo hakikisha umeyavunja malengo yako katika hatua
ndogo ndogo ambazo unaweza kufanya kila siku. Ukiweza kufanikisha mpango wa
kwanza nenda kwenye mpango unaofuata. Jinsi unavyoweza kufanikisha malengo yako
ndivyo zaidi unavyopata msukumo wa kufanya zaidi.
3.
Kubali, Ongea na Chukua Hatua
Kwa Vitendo Kwa Yale Unayoyaamini
Ukitaka kufikia mafanikio
makubwa kwenye maisha yako ni lazima ufunge mlango wa mawazo yako dhidi ya
mambo yote yanayoweza kukukatisha tamaa. Kama utakuwa umefanya uchunguzi kwenye
maisha yako ni kwamba utagundua siku zote kama unataka kufikia ndoto kubwa
utaona kama akili yako inakwambia kwamba haiwezekani. Lakini ukweli ni kwamba
kama unataka mafanikio makubwa ni lazima uende maili ya ziada isiyo ya kawaida.
Lazima uiambie akili yako kwamba inawezekana. Zaidi unavyojenga Imani ndivyo
hivyo unavyoweza kuondokana na hofu ya kushindwa. Wewe ndiye wa pekee unayeweza
kujihamasisha kufikia mafanikio yako na tambua kwamba hawezi kutokea mwengine.
4.
Tenda Kwa Ujasiri Na Uadilifu
Uadilifu ni muhimu sana kama
wewe ni mfanyakazi au mwajiri, mwanfunzi au mfanyabiashara. Uadilfu lazima uwe
mzima usiogawanyika, uwe na uwezo wa kuzalisha matokeo sawa bila ya kujali
mazingira gani uliyopo. Lazima ukuze maadili ya uaminifu na maadili yaliyo
imara. Siku zote ukiwa muadilifu basi ujasiri hufuata.
5.
Fanya Ukaguzi Wa Kila Kitendo
Kila hatua lazima iwe na
matokeo. Hivyo pima kitendo chako cha kabla na baada ya wewe kufanya ili kujua
hasa athari ya tendo juu ya maisha yako na mafanikio. Jambo muhimu la kukumbuka
katika vitendo vyako ni kwamba kila kitu kina umuhimu na kila kitendo lazima
kilete matokeo.
Unapoweza kupanga mlengo yako
kwa kiwango cha juu, unapochukua hatua ya kufanya mambo makubwa, Unapoweza
kutenda kwa ujasiri na uaminifu na ukiweza kufanya ukaguzi wa kila tendo
unalotaka kulifanya basi utakuwa umeweza kupata mafanikio makubwa kwenye maisha
yako.
Weka email yako hapa na bonyeza
Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
0784498867
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena