Kila mtu duniani ana utaratibu wake wa maisha. Ili kuweza kuishi maisha yako ya pekee usikubali kufuata watu wanavyotaka wewe uishi. Ni muhimu kujipangia utaratibu wako utakaoufuata na kukuwezesha kuishi vizuri.
Zifuatazo ni kanuni zitakazokuwezesha kuishi maisha yako:
1. Jifikirie wewe kama wewe
![]() |
Kwa Nini Nafanya |
Usikubali kila kitu unachoambiwa. Unapoambiwa kitu lazima uhoji na kufikria kwa umakini ndipo ufanye maamuzi. Unapofikiri kwa umakini kutakusaidia kupunguza kujuta na mawazo yasiyo ya lazima.
![]() |
Watu Wananionaje |
Mtazamo wako ndio uko sahihi. Usijaribu kufuata kila kitu kutoka kwa watu. Fanya unayoyaamini . Yale unayoyaamini ndiyo yanayokufanya wewe uwe na mtazamo na maamuzi yako.
![]() |
Kushindwa Sio Mwisho Wa Maisha |
Fahamu unachokitaka. Tengeza maisha yenye muelekeo ambao utafika kule unakotaka kufika.
4. Furahia Kazi Zako.
![]() |
Furaha Ndio Kazi Yangu |
Usikubali furaha yako iishie kwenye mikono ya watu wengine. Jipende mwenyewe na fanya kila kilicho kizuri kwa maisha yako. Jione kwamba wewe ni wa muhimu kuliko mtu yeyote kwenye maisha yako.
![]() |
Siogopi Changamoto na Najiamini |
Jiamini. Chochote unachofanya fanya kwa kujiamini. Sema ukweli wakati wote ili uweze kujenga Imani ya kujiamini.
![]() |
Haya Mambo Hayakuhusu |
Usiwe mtu wa kushughulikia mambo yasiyokuhusu. Muda mwingi kuwa karibu na kazi zako na wala usifanye vitu ambavyo havina faida kwako.
![]() |
Ni Wakati Wa Mapambano |
Usikae kimya, uliza kila kitu. Tafuta taarifa, soma sana na fanyia kazi kila hatua unayojifunza.
![]() |
Chagua Njia Yako |
Hakikisha kila jambo unalolifanya unafanya kwa kujitofautisha na wengine. Fuata taratibu na kanuni zako ulizoweka. Fanya kitu ambacho hakuna mtu yeyote anaweza kukifanya.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena