Watu wengi wanapenda kuanzisha
blog kwa mtindo wa kuiga. Unapoanzisha blog kwa kuiga na kuchukua kazi za watu
wengine ni kwamba blog yako haitoweza kufika mbali. Ili Kuifanya blog
yako iwe ya tofauti inawezekana ingawa inahitaji muda.
Ili kuifanya blog yako iwe ya
tofauti na kuifanya iwe na mafanikio makubwa unahitaji kufuata hatua zifuatazo:
1. Anzisha
Blog. Kama bado hujaanzisha blog anza leo. Kuanzisha blog ni bure huhitaji
gharama yoyote ile kwa kuanzia. Zipo baadhi ya blog ni za kulipia lakini pia
zipo za bure. Unaweza kuchagua moja kati ya hizi. WordPress, Blogger, Tumblr,
Medium, Weebly na nyengine nyingi.
2. Chagua Mada ambayo unayoipenda.
Hakikisha unachagua mada unayoipenda. Watu wengi wanapenda kusoma mambo
yanayoweza kutatua changamoto zinazowakabili. Blog yako itakuwa ya tofauti
sana ukiweza kuandika makala ambayo yataweza kutatua matatizo yao. Ukiweza
kuandika makala kwa kuweka na picha utaifanya blog yako ivutie zaidi.
hivyo kuifanya blog yako kuwavutia wasomaji wengi.
3. Soma
Sana. Unahitaji kusoma vitabu sana. Unahitaji kupitia blog za watu wengine
ili kuweza kujifunza mbinu za kiuandishi na uzoefu wa watu wengine.
Lazima kila siku uwe mwanafunzi wa kuwa tayari kujifunza.
4. Fanya
Ubunifu Kwenye Blog Yako. Hakikisha blog yako inakuwa ya kisasa kwa kufanya
ubunifu wa templeti yenye kuvutia na yenye kushawishi wasomaji. Ifanye iwe
rahisi na yenye kueleweka kwa kuzingatia ubunifu wa kitaalamu. Ifanye blog yako
iwe ni rahisi kuonekana. Hii inawezakana kwa kutengeneza maneno ambayo yatakuwa
na urahisi wa kuonekana. Ifanye mtu akitafuta basi iwe ni rahisi kuiona blog
yako. Fanyia ubunifu kutokana na mahitaji ya msingi ya watu.
5. Onesha
muendelezo wa makala zako. Hakikisha unatuma taarifa kila siku. Unapotuma
taarifa kila siku ni rahisi blog yako kutambulika na kupata watembeleaji
wengi. Vile vile kama blog yako itatoa vitu ambavyo watu wanavitafuta ni
rahisi kwako kubaki kwenye ubora na kuendelea ukuaji wa blog yako.
6. Bakia
Kwenye Mada. Kama unaandika kuhusu mafanikio basi baki kwenye makala
za mafanikio. Kama hutoweza kubaki kwenye mada ni rahisi kuwapoteza wageni
wanaotembelea blog yako.
7. Fanya Makala Za Kipekee. Hakikisha
makala zako hazipatikani kwenye blog nyengine. Jaribu kubadili utaratibu watu
waliouzoeya. Pangilia makala zako. Jinsi unavyoweza kupangilia kazi zako ndivyo
hivyo hivyo blog yako itakavyoonekana kuwa na muonekano mzuri.
Hakikisha kila siku unatuma
mambo yanayowashangaza watu.
8. Tangaza Blog yako. Ukiweza
kufikisha makala kumi na tano( 15) anza kuitangaza blog yako. Zipo njia nyingi
za kutangaza blog yako.
- Weka
taarifa zako kwenye mitandao ya kijamii.
- Weka
vichwa vya habari vionekane kwenye Google
- Badilishana
link ya makala zako na blog nyengine.
9. Kuwa karibu na wasomaji
wako. Msomaji wa blog yako anapouliza maana
yake ni kwamba anahitaji maelezo. Usidharau hakukisha unampatia majibu yenye
kuridhisha.
10. Wajue wasomaji wako. Ni muhimu
kujua wasomaji wako wanapenda nini. Hakikisha unafanya blog yako iwe na vitu
ambavyo wasomaji wako watajifunza na kufaidika kwa uwepo wa blog yako.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena