Jumatano, 19 Oktoba 2016

Zijue Faida Tano (05) Za Kutumia Muda Wako Vizuri Unapokuwa Peke Yako


Unapotumia muda wako kwenye mazingira ambayo hakuna muingiliano na kelele za watu huwa unakuwa na uhuru mkubwa wa kufikiri na kufanya kazi zako kwa mafanikio makubwa.

Zipo faida nyingi za matumizi ya muda  ukiwa peke yako. Na hizi hapa ni baadhi ya faida unazoweza kuzipata kwa kutumia muda wako ukiwa peke yako.

1.           Unapotumia Muda Ukiwa Peke Yako Kutakufanya Uweze Kujiamini
Watu wengi ambao hawajiamini wanategemea msaada kutoka kwa watu wengine. Lakini unapoweza kuutumia muda ukiwa peke yako unakuwa na moyo wa matumaini wa kufanya maamuzi yako. Unapokuwa peke yako ni rahisi kutumia mawazo yako kwenye kufanya maamuzi. Unapokuwa peke yako ni rahisi kupima faida na hasara kwenye lile eneo ulilokusudia kulifanya. Na hii inaweza kujenga uwezo wa kujiamini kufanya pasipo na kumtegemea mtu.

2.           Kutumia Muda Ukiwa Peke Yako Kutakuongezea Uzalishaji
Mara nyingi tunapozungukwa na watu wengine, tunakuwa na hofu ya kufanya malengo na mipango yetu. Unapokuwa peke yako unakuwa na muda wa kutosha kufikiria kazi yako na mambo yako ya msingi. Na hii inatusaidia kuamua kutekeleza malengo yetu na kuweza kuzifikia ndoto zetu.

3.           Unapotumia Muda Ukiwa Peke Yako Kutakusaidia Wewe Uweze Kuwa Mbunifu
Kila mtu ni mbunifu kwa njia yake anayoijua, lakini unapozungukwa na watu tofauti ni rahisi kufanya kile ambacho watu wanafanya. Unapoweza kuwa peke yako ushawishi wa watu unakuwa haupo. Na hiyo itakusaidia kufanya kitu ambacho ni cha kwako. Ukiwa peke yako unapata nafasi ya kufanya kutokana na uwezo wa akili yako.

4.           Unapotumia Muda Ukiwa Peke Yako Unaweza Kusafisha Akili Yako
Jamii yetu imetawaliwa na taarifa nyingi. Mara nyingi akili zetu zinajazwa taarifa kutoka kwenye kazi, mitandao, marafiki na hata familia. Kutumia muda ukiwa peke yako unaruhusu akili yako iwe safi, ambayo itakufanya kuwa na furaha na kuweza kutuliza mawazo.

5.           Kutumia Muda Peke Yako Kutakusaidia Kutatua Matatizo
Njia bora ya kutatua matatizo inakuja pale ambapo unakuwa na uhuru wa kuwa peke yako. Kutumia muda ukiwa peke yako kutakusaidia kuwa na uwezo wa kufikiria matatizo na njia sahihi za kutatua matatizo. Kuwa peke yako inarahisisha uwezo wa kufikiria chanzo cha tatizo na njia tofauti za kushughulikia tatizo. Na vile vile kuwa peke yako ni muda mzuri wa kufikiria fursa zinazokuja kwako.

Muda mzuri wa kuweza kupata faida nilizozitaja wa kuwa peke yako ni wakati wa asubuhi. Asubuhi ni wakati ambao utulivu wa hali ya juu unapatikana. Hivyo nakushauri ndugu msomaji wa Makala hii hakikisha unaamka kila siku asubuhi mapema kabla ya dunia haijaamka. Tumia muda huo kutafakari mambo mbali mbali ya msingi kwa faida ya maisha yako.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA