Jumanne, 18 Oktoba 2016

Mambo Matatu (03) Muhimu Unayotakiwa Kupunguza Kuyafanya Kuanzia Leo Kama Unataka Kuishi Maisha Ya Mafaniko


Ni ukweli usiopingika kwamba tunaishi katika dunia iliyojaa kila kitu. Tumekuwa wa kupoteza muda mwingi kufanya na kuangalia mambo yanayo tupotezea muda wetu. Kuachana na mambo yasiyo na umuhimu katika maisha yetu sio tu yanaturahisishia maisha yetu lakini vile vile tutaifanya akili yetu iwe na nafasi ya kutosha kwa ajili ya kufanya vitu vyenye maana na kuishi maisha mazuri. Kuachana na mambo yasiyo na msingi tunaipa akili uwezo wake wa kufikiri.

Haya hapa ndio mambo matatu ya kujifunza yanayotoa nafasi ya kuishi maisha rahisi na yenye furaha kwa ajili ya mafanikio yetu:

1.           Punguza Muda Wa Kuangalia Luninga
Tunatumia muda mwingi wa kushughulika na kuangalia vipindi kwenye luninga. Mara nyingi uzoefu unatuonesha ukiwa na tabia ya kuangalia luninga unaweza kuishia kuupoteza muda mwingi hufanyi mambo ya msingi na  badala yake unatumia muda huo kuwa kwenye kioo cha luninga. Kuangalia sana luninga kuna athari ya kutumia muda vibaya. Muda ambao ungeweza kuutumia katika mambo ya uzalishaji na ukaweza kuleta mafanikio makubwa.

2.           Punguza Kuongea Maneno Matupu
Hii sina maana kwamba usiache kuongea. Maana yangu ni kwama ni muhimu  kuangalia maneno unayo yasema. Maneno unayoyasema lazima yawe chanya. Maneno yawe yenye kuaminika na yenye kuleta maana. Kusema maneno machache yenye ubora ni njia mzuri  zaidi kuliko kusema maneno mengi yasiyo na ubora.

3.           Punguza Muda Wa Kuangalia Mitandao Ya Kijamii
Kutokana na nguvu ya utandawazi  katika ulimwengu wa sasa, mitandao ya kijamii imetufanya kuzitawala akili zetu. Rahisisha maisha yako  kwa kupunguza kuangalia mitandao ya kijamii. Tumia muda mchache kwa kuangalia yale ambayo unaweza kujifunza na achana kabisa na mambo ya kufurahisha yasiyokuwa na faida katika maisha yako.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA