Kila mtu anaweza kuleta tafsiri ya
mafanikio kutokana na mtazamo na uelewa wake. Kwenye mafanikio yapo mambo ya
msingi kwa kila mtu ambayo akiendelea kuyafanya yanaweza kuwa ndio sababu ya
yeye kufanikiwa. Vile vile kuna mambo ambayo mtu akiendelea kuyafanya
yanaweza kuwa ndio sababu ya yeye kutoweza kufanikiwa. Binaadamu tunao
uwezo mkubwa wa kuzuiya mambo yanayokwamisha mafanikio yako.
Yafuatayo ndio mambo yanayo kwamisha mafanikio
yako:
1.
Kutengeneza Visingizio
Kutenngeneza visingizio ni ile hali ya
kila wakati hukosi sababu. Wewe unakuwa ni mtu wa kulaumu watu kwa sababu
hujatimiza kile unacho kitaka. Acha kukataa majukumu yako pale unapofanya
makosa. Kama umeshindwa hadi leo kufanikwa kwa sababu ya uchaguzi wako wa
kimaskini, huna sababu ya kifikria mafanikio uliyoyakosa kwamba yako nje
ya uwezo wako. Naomba nikwambie kwamba watu wenye mafanikio hawafanyi hili
kosa. Usipoteze muda kwa kutengeneza visingizio kwa yale mambo ambayo
umeshindwa kuyafikia. Visingizio havitokusaidia kufikia mafanikio.
2.
Mtazamo Hasi
Kama unataka kuvuna mafanikio ya maisha
yako unahitaji kuangalia mambo mazuri. Usitoe nafasi ya kufikria vitu
hasi kwenye maisha yako. Muda wote kuwa na mtazamo chanya. Mtazamo chanya
hauwezi kuleta mafanikio ya maisha yako.
3.
Kuogopa Kufeli
Huna sababu ya kuogopa kufeli.
Kufeli kwako iwe ni msingi wa kujifunza na kuchukua hatua. Unapofanikiwa
unaelewa kuwa umefanya vizuri. Unapofeli unaona kama umefanya vibaya na
kujisikia vibaya. Ingawa kufeli kunaumiza lakini kama unataka mafanikio ni
lazima uwe na mtazamo wa kufeli kama fursa ya kuelekea mafanikio.
4.
Kukata Tamaa
Unapokutana na vikwazo vya maisha usikate
tamaa. Watu waliofanikiwa hawakati tamaa. Waliofanikiwa wanajitoa ili waweze
kufika safari yao. Hawaruhusu vikwazo viwafanye wasiweze kujaribu tena.
Msingi mkuu wa mafanikio ni kujaribu kwa uwezo wako. Kama utaweka juhudi
zako zote kwenye eneo unalolifanya bila ya kumuathiri mtu basi wewe utakuwa ni
mtu uliyefanikiwa.
5.
Kuangalia Njia Nyepesi
Kwenye mafaniko hakuna njia ya mkato.
Unatakiwa kujipa changamoto ya kufanya vitu vilivyoshindikana. Jivute hadi
mwisho wa uwezo wako. Weka lengo la kufikia uwezo wako wa mwisho, na nenda
zaidi ya hapo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena