Jumapili, 16 Oktoba 2016

Funguo Tatu (03) Za Mafanikio Ya Maisha Yako


Tatizo kubwa kwenye dunia tunayoishi leo ni watu kukosa ufahamu wa maisha. Watu wengi wanaishi kwa kufuata mkumbo. Tunaishi maisha ya kuiga na kuingia kwenye mtego wa kuishi maisha yasiyo na muelekeo. Tumekuwa tukiishi kwa kutumia muda mwingi kwa kufuata mazingira. Tufanya kile kinachotutokea ambacho hatujapanga kukifanya. Tumesahau kubaki kwenye malengo na mipango yetu.

Kuwa na ufahamu na kuchukua  maamuzi kwa usahihi ya kuishi maisha yako ya kila siku kwa vitendo kutakuwezesha kufikia malengo yako uliyojiwekea. Ishi kwa kuzingatia  madhumuni ya maisha yako. Fanya kutokana na thamani yako na usiwaruhusu watu wakuamulie nini cha kufanya.
Unapoamua kufanya maamuzi ni lazima kwanza kufikiri kama hayo unayoyafanya yanakupelekea kufika kwenye malengo yako.
Kama kweli unahitaji kufikia mafanikio ya uhakika. Ni muhimu kufuata funguo hizi tatu zitakazokufanya uishi kwenye maisha ya mafanikio:

1.           Andika Malengo Yako.
Kitu cha kwanza unachokifanya asubuhi unapoamka ndicho kitakacho onesha mwelekeo mzima wa siku yako. Andaa mpango kwenye akili yako ambao utakupa nguvu mara unapoamka na amua kufanya.
Hakikisha unafanya hivyo kwa kuyaandika malengo yako kila siku asubuhi. Baada ya kuandika weka alama kwenye lile lengo muhimu kuliko yote. Lengo ambalo ni la muda mrefu ndilo litakalokuwa na thamani kubwa kwenye maisha yako. Baada ya hapo jiulize “Ni hatua zipi naweza kuchukuwa leo ambazo zitaweza kukuweka karibu na kuyafikia malengo yako”.  Andika hatua zote unazoweza kufikiria na zichague mbili ambazo ni za muhimu zaidi. Ukishazichagua anza kwa kuzifanyia kazi kwa vitendo. Hakikisha huachi kufanya mpaka zikamilike. Hii ni hatua muhimu sana ya kufanya mara unapoamka. Kufanya hivyo kutaifanya kili yako iwe ni yenye kuzalisha.
Sababu nyengine ya kuyaandika malengo yetu ni kwamba unapoyaandika inakufanya kila siku uweze kuyasoma. Na ukiweza kufanya hivyo utajisikia vizuri sana. Mtindo wa kuyaandika ni ule wa kama tayari umeshayafikia. Yasome na kuyarudia kila siku asubuhi ili uweze kubaki kwenye malengo yako. Kumbuka malengo ambayo hayapo kwenye maandishi ni vigumu kuyafikia.

2.           Tengeneza Mfumo Unaoweza Kuuamini.
Jiamini wewe kwanza na amini kile ambacho unakwenda kukifanya. Kama ukishindwa kijiamni hakuna atakaye kuamini.
Kama kuna mtu atatokea kukuuliza kuhusiana na malengo yako ya maisha, usiogope kusema. Hakikisha unasema kwa sauti yenye kujiamini. Ikiwa leo hii atokee mtu akuulize kuhusu lengo lako la maisha halafu utoe jibu la sijui basi wewe utakuwa ni mtu wa kushangaza sana.
Hatua muhimu ya kuishi na kufanikiwa kwenye ndoto zako ni kuamini kile unachofanya. Ukiweza kuamini kwenye akili yako kwamba tayari umefanikiwa malengo yako utakuwa umejenga hisia za uhakika. Uhakika ambao utakusaidia kufanya kwa vitendo. Ukiweza kufanikiwa kujenga mfumo wa uhakika utakuwa unakaribisha kuyapata mafanikio kwa urahisi zaidi. Ukiweza kutengeneza mfumo wa twasira inayojirudia rudia kwenye akili yako utakuwa umetengeneza nguvu ya kuyafikia mafanikio.

3.           Wekeza Wewe Mwenyewe.
Vitu ambavyo unaweza kuvifanya kwa ajili ya uwekezaji huu ni kama vifuatavyo:
  • Fanya Mazoezi. Unapofanya mazoezi unaimarisha mwili wako uwe na nguvu za kutosha kuweza kuzalisha zaidi.
  • Kula Vizuri. Kula chakula chenye afya kila siku kutausaidia mwili wako uwe na afya njema.
  • Anza Kusoma Vitabu. Hakikisha unasoma vitabu vya kutosha. Unapoamua kusoma hakiksha unaondoka na kitu cha kujifunza.
  • Andika. Usiruhusu kuondoka nyumbani bila ya kuwa na kalamu na karatasi. Wazo lolote linalokuja kwenye akili yako hakikisha unaliandika muda huo huo. Usiamini akili yako kama ndio itaweza kukumbuka kila kitu.
  • Jifunze Ujuzi Mpya. Kila siku hakikisha unajifunza kitu kipya. Kitu kimoja kipya unachojifunza kwa siku moja ni sawa na vitu 365 utakavyojifunza kwa muda wa mwaka mzima.

Ushauri wangu wa mwisho ambao naweza kukupa kwa leo ni kwamba hakikisha unaenda mbele. Rudia malengo yako na fuata funguo hizi tatu za mafanikio ya maisha yako.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA