Jumamosi, 15 Oktoba 2016

Zifahamu Tabia Nane (08) za Watu Wenye Hamasa za Kipekee.



Watu wenye mafanikio makubwa wanakuwa na hamasa ya mafanikio. Fahamu siri zao na zifanyie kazi ili na wewe uweze kupata mafaniko.

 


Watu wenye hamasa za kipekee wanalazimika kufanya zaidi kuliko kawaida. Watu hawa ni watu wenye heshima na kuaminiwa na wengine. Ni watu wanaojiamini kwa kila kitu wanachofanya. Maisha yao na ndoto zao zinakuwa hazina mipaka na wanaridhika na maisha yao.

Hawa ni watu ambao mtazamo wao huwa ni ushindi daima, shauku ya mafanikio, na wanafanya mambo ambayo huwafikisha kwenye safari yao ya mafanikio.

Hizi hapa ndio siri zao zinazowahamasisha kuyafikia mafanikio ya kipekee:

1.           Wanakuwa na Hamasa ya Ndani.
Wanakuwa na nguvu ya ndani inayowasukuma kuanza safari mpya, kuleta matokeo mazuri  na kuweza kutatua changamoto zao.

2.           Hawana Muda wa Kupoteza Kwenye Malumbano.
Mara zote huwa wanaona mafanikio na makosa ya wengine kama silaha ya kujifunza badala ya kuanzisha hoja za kulumbana.  Hawana muda wa kugombana wala kuanzisha mambo ambayo hayana tija kwenye kuwaletea mafanikio.

3.           Wanakuwa na Nidhamu.
Wanapofanya makosa wanakuwa tayari kukubali makosa yao na kuomba msamaha . Wanakuwa na moyo wa kuwapa hamasa wengine na kushauri njia za kufanya zitakazowaletea mafanikio.

4.           Wanakuwa Wakweli.
Wanakuwa ni watu wenye mtazamo wa kweli. Hawaishi kwa sababu ya kuwafurahisha wengine. Ni watu wenye kuwa na misimamo ya kweli na wala hawayumbishwi na wengine.

5.           Wanakuwa na Mtazamo wa Mafanikio.
Watu hawa wana tabia ya kufanya yale maeneo yenye kufanya kazi na yanayoweza kuwaletea mafanikio. Hawaangalii historia mbaya bali wanaangalia mambo yaliyonyooka na yenye mtazamo wa mafanikio.

6.           Wanafanya Zaidi Kuliko Kawaida.
Watu hawa wanaangalia mambo magumu kuweza kupata kile wanachokitaka na wala hawachagui maeneo mepesi . Wanafanya mambo ambayo hakuna mtu anayetegemea kuyafanya. Wanaamini uwezo wao na wanakuwa na uhakika wa kufanikiwa.

7.           Wanaendelea Kujifunza.
Wanasoma sana na siku zote wanatafuta taarifa mpya kwa umakini mkubwa. Ni watu wanaoelewa kwamba ili uweze kukua ni lazima kujifunza.

8.           Wanafahamu Wanachotaka.
Mtazamo wao upo sahihi kuhusiana na kile wanachokitaka kwenye maisha na wanakuwa tayari wanajua ni wapi wanata kufika. Ni watu wasioruhusu kushindwa na mtazamo wao wanaamini kwamba kila kitu kinawezekana.

 
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA