Ijumaa, 14 Oktoba 2016

Fahamu Mambo Manne (04) Yatakayokusaidia Kutambua Uwezo Wako.


Karibu tena ndugu msomaji wa Makala hii. Leo nataka nikuelezee mambo yatakayokufanya uwe na maisha bora. Mambo nitakayokueleza yatakufanya ubaki  kwenye njia ambayo unaweza kuwa na uwezo nayo na kupelekea maisha yako kuwa bora siku zote.

Kwenye kazi yoyote unayoifanya kuna uzaifu na uimara. Hivyo ni vyema kufahamu uzaifu wako upo wapi na uimara wako ulipo. Ukiweza kugundua wapi ndipo una nguvu zaidi hapo ndipo kwenye maisha yako ya  mafanikio. Kama bado umeshindwa kujua nguvu zako zilipo hakikisha unajitoa  katika kutafuta na uweze kukundua nguvu zako zilipo. Ukiweza kujua wapi unaweza kuwa bora hakikisha unabaki hapo. Kama bado unashindwa kujua nguvu zako zilipo wapi usiwe na wasiwasi endelea kufanya kazi kwa bidii. Unapofanya kazi zaidi ndipo unapogundua uimara wako ulipo.

Mambo yafuatayo yatakusaidia kuweza kufahamu uwezo wako na kipaji chako:

1.           Jiulize ni wapi unafanya vizuri.
Jiulize ni maeneo gani unaweza kufanya vizuri. Ukijua ni wapi unaweza kufanya vizuri na kwa usahihi basi tumia nguvu hizo ufanye kwa bidii hadi ufikie sehemu mzuri ya maisha yako.

2.           Kuwa Wazi.
Uwezo wako siku zote huwa uko wazi. Jinsi ambavyo utakuwa muwazi na kufanya kwa umakini ndivyo hivyo utakavyoweza kuona uwezo wako ulipo.

3.           Sikiliza Watu Wengine  Maeneo Wanayokusifia.
Sikiliza wengine wanasema nini kuhusu wewe. Uwezo wako unaweza kuufahamu kupitia kwa watu wengine. Sikiliza kwa umakini yale wanayoyasema na fuatilia. Unapofanya kazi kwa kiwango hafifu hakuna ambaye atafurahishwa na kazi zako. Lakini unapofanya kazi kwa uwezo wako watu watakusifia . Eneo ambalo umekuwa ukisifiwa endeleza na huo ndio uwezo wako.

4.           Angalia Watu Waliokuzunguka.
Huhitaji kupoteza muda mwingi kujilinganisha wewe na wengine. Unapojilinganisha wewe na watu waliokuzunguka unatakiwa kujiuliza kwamba wao wanafanya kama wewe unavyofanya. Watu waliokuzunguka wanafanya vizuri kuliko wewe. Unapojiuliza masuali ya kufanya vizuri kuliko wengine itakusaidia kuweza kuwa wa tofauti na wengine. Tafuta kitu kinachokufanya uwe tofauti na wengine. Endelezea hiyo tofauti yako mpaka ufikie uwezo wako.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA