Alhamisi, 20 Oktoba 2016

Hizi Hapa Ndio Sababu Sita (06) Za Kwa Nini Watu Wanaotumia Muda Wakiwa Peke Yao Wanakuwa Na Mafanikio Makubwa


Watu wengi katika jamii tunayoishi wanapenda kufanya vitu kwa kujionesha. Mara nyingi imetokea watu wakiyakosa mafanikio kutokana na kufanya vitu kwa kujionesha kwa marafiki. Ni vyema kama una mipango yako usiruhusu kuharibiwa na wengine kwa kuwashirikisha mwanzoni kabla ya kufika safari yako. Unapotumia muda wako kwa kuwa  peke yako  kutakuwezesha kutumia muda wako vizuri kwa faida ya mafanikio yako.

Watu waliofanikiwa wameweza kuzitumia sababu hizi na kuwaletea mafanikio makubwa:

1.           Wanakuwa Hawana Wasiwasi
Watu waliofanikiwa waliweza kuutumia muda wao kwa kukaa peke yao. Kukaa peke yako kunakufanya ufanye kazi zako kwa umakini wa hali ya juu. Wakati wa kuwa peke yako unaruhusu mawazo yako yabaki kwenye mtazamo chanya.

2.           Wanakuwa na Kumbukumbu Mzuri
Unapokuwa peke yako unakuwa na uwezo wa kujenga kumbukubu mzuri katika akili yako. Kuwa peke yako unapata kipimo kilicho sahihi cha kugundua uwezo wako katika kufanya maamuzi sahihi.

3.           Wanajielewa Wao Ni Nani
Ukweli ni kwamba umezaliwa ukiwa wa pekee na utakufa ukiwa wa pekee. Na hii ndio sababu wewe unatakiwa ufanye mambo yako ya aina ya pekee. Huna sababu ya kujilinganisha na watu wengine. Mafanikio yako utayapata kwa kuweza kujitambua wewe ni nani katika maisha yako.

4.           Wanakuwa Na Mahusiano Mazuri
Muda unaokaa peke yako unapata ufahamu wa kujielewa wewe na kuwaelewa vizuri waliokuzunguka. Kukaa peke yako inakusaidia kujua mahusiano yako na wengine na hatua mzuri za kuchukua kuweza kukuza mahusiano hayo.

5.           Wanakuwa Na Uwezo Wa Kufanya Maamuzi Sahihi
Upweke unakupa fursa ya kufikiri kupitia kila kitendo unachofanya. Unaweza kuwa tayari kusimama kwa ajili ya kitu chochote unachotaka kufanya mwenyewe. Upweke hukusaidia kupata sauti yako mwenyewe.

6.           Wanakuwa Na Ufahamu Wa Mambo Ya Maisha Kirahisi
Kuwa peke yako kunakufanya kuyaona maisha kutokana na mtazamo wa wazi. Kuwa peke yako kunakupa upeo wa kuangalia mambo kwa njia iliyo nyepesi na rahisi kufahamika. Ni rahisi kufanikiwa kama kila kitu kwako unakifanya kwa njia ambayo haina kona nyingi.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA