Katika jamii tunayoishi
tumezungukwa na watu tofauti tofauti. Wengine ni marafiki lakini pia wengine ni
maadui zetu. Mahusiano ni moja kati ya changamoto zinazotukabili katika
maisha yetu ya kila siku. Wapo watu wanaoweza kukuunga mkono kwa mambo
unayoyafanya lakini pia wapo wanaojenga chuki kwa hatua unazopitia.
Kipimo kizuri cha mafanikio ya
maisha ni kuishi na watu vizuri. Unapoweza kuishi na watu vizuri utajenga tabia
ya upendo kwa watu. Yapo mambo mengi mazuri tukiyafanya yanatupeleka kwenye
kujenga mahusiano bora. Fahamu kwa kujenga mahusiano kwenye jamii ni jambo
lenye maana sana kwa mafanikio yetu ya leo na kesho.
Katika Makala hii nitataja mambo
mawili miongoni mwa mambo mengi ambayo ukiyafanya yatakusaidia kujenga
mahusiano mazuri katika jamii. Na unapojenga mahusiano hayo unakuwa umefungua
milango ya mafanikio yako.
1. Kubali tofauti zilizopo
katika jamii
Tambua kwamba binadamu
tunatafautiana kwa tabia. Tofauti zetu ni haki ya msingi kwa kila mtu. Hivyo unapoamua
kujenga mahusiano na watu waliokuzunguka, usimuhukumu mtu kwa makosa anayofanya
kutokana na kutofautiana kauli au mtazamo. Si lazima kupenda yale mambo
wanayofanya wengine lakini tusijenge tabia za chuki kutokana na yale
wanayofanya wengine. Tusiruhusu akili zetu zipoteze muda kwa kufikiria kwamba
ni kitu rahisi kuzifanya akili za wengine ziendane na vile unafikiria wewe. Ni
kitu kisichowezekana watu wote kuwa na tabia zinazofanana.
2. Jenga Tabia Na Mwenendo
Utakaopendwa Na Watu
Binaadamu anatakiwa aishi kwa
kuzingatia tabia na mwenendo wake mzima wa maisha. Tabia nzuri ndio msingi wa
mafanikio ya kila mtu. Kumbuka tunatakiwa tutende wema, tuwe wacheshi, tuwe
waadilifu ili tuweze kujenga mwenendo na kuonesha haiba nzuri ya tabia.
Tengeneza mazingira yatakayoweza kujenga umoja na udugu kwa watu wako
waliokuzunguka. Iwe ni kwenye kazi, majirani na hata watu unaoweza kukutana nao
mara kwa mara. Kufanya hivyo kutakusaidia kujenga mahusiano mazuri na hali hiyo
itakusaidia kufikia ndoto zako za mafanikio.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena