Katika Makala hii nitaendelea
kuelezea mambo mengine miongoni mwa mambo ambayo ukiyafanya yatakusaidia
kujenga mahusiano mazuri katika jamii. Na unapojenga mahusiano hayo unakuwa
umefungua milango ya mafanikio yako.
Haya hapa ndiyo mambo ambayo
yanaweza kukujengea mahusiano mazuri na watu:
1. Wape Watu Nafasi Ya Kuongea
Unapotoa nafasi kwa watu ya
kusikiliza na kuheshimu kile anachokiongea humfanya mtu huyo ajisikie amepewa
heshima ya pekee. Kama unataka kujenga mahusiano mazuri na watu wengi ni muhimu
kuwapa nafasi ya kuongea na wewe. Hakikisha unawapa muda wa kutosha wa
kusikiliza maoni yao na mwisho wawekee mazingira ya kuthamini mchango wao.
2. Wafanye Watu Wajione Wana
Thamani Ya Hali Ya Juu
Wafanye watu wajione wako juu.
Usipende kabisa kuwadharau kwa mapungufu walionayo. Onesha ushirikiano na haki
sawa kwa wote. Unapozungumza nao jenga tabia ya kuwaheshimu na kuwathamini.
Tabia hii huwafanya wakuone una thamani kubwa kwao na hii itakufanya mahusiano
yenu yachanue.
3. Usiwalaumu Watu Kama Kuna
Tatizo Limetokea
Ni kawaida kwa watu wengi
kutanguliza lawama mara tatizo linapotokea, kufanya hivyo mara nyingi tumeona
kuvunjika kwa mahusiano. Kumbuka hakuna jambo linalovuruga upendo na mahusiano
kama kulaumiana. Epuka kabisa kutumia lawama kama silaha yako kuu ya kuwahukumu
watu wanapofanya makosa, badala yake ni vyema kutafuta chazo cha tatizo na
kuangalia njia nzuri ya kutatua tatizo hilo pasipo na kuanza lawama. Hutoweza
kudumu na ushirika mzuri wa mahusiano kama utatanguliza lawama.
4. Tuwapime Watu Kwa Mtazamo
Chanya
Unapoamua kujenga mahusiano na
watu hakisha unawapima kwa mtazamo chanya. Unapompima mtu kwa mtazamo hasi
unamfanya ajisikie vibaya na kuhisi amedharauliwa, matokeo yake unakuwa
umepunguza thamani ya mahusiano yenu. Ikitokea mtu huyo kuwa na mapungufu
kwenye jambo lolote basi hakikisha unamueleza kwa lugha yenye kumsaidia aweze
kurekebisha. Kufanya hivyo utamfanya ajisikie vizuri na kupelekea kudumisha
mahusiano yenu.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena