Watu wengi wanafikiri kuwa wa
tofauti ni jambo lenye mtazamo hasi. Lakini hivyo sivyo ilivyo. Kuwa wa tofauti
ni sehemu ya maisha.
Utofauti ninaouzungumzia hapa ni
yale maamuzi ya kuwa mbishi. Au kwa lugha nyepesi ni kupinga au kwenda kinyume
na watu wanavyotarajia. Wanaweza wakakuita mpinzani kwa yale mambo ambayo
wamezoeya kuyafanya.
Hapa naweza kutoa mifano ya
maamuzi ya msingi ambayo yanapelekea kuwa wa tofauti kwa wengine.
1.
Kuacha kazi yako ya kuajiriwa
uliyoizoeya na kwenda kufanya biashara.
2.
Kuacha chuo na kwenda kuanzisha
biashara.
3.
Kuondoka sehemu ya mji
uliozaliwa na kwenda sehemu nyengine kutafuta maisha.
4.
Kufanya vitu kinyume kabisa na
vile kila mtu anafanya.
5.
Kuazisha jambo ambalo halijawahi
kufanywa.
Ni kawaida kwa watu wanaofanya
vitu tofauti kuwasahihisha wale wafanyao makosa. Na wanapofanya hivyo ndivyo
wanapotengeneza maadui, washindani na hata kuchukiwa na wengine. Mwisho
kutamani bora kuondoka duniani.
Kuna methali isemayo “ Mwenye
mafanikio ni yule ambaye hujenga msingi wake wa matofali lakini wengine
wanakuja kuubomoa’’.
Tukirudi kwenye historia kuna
watu mashuhuri duniani ambao walifanya vitu tofauti. Hawa walifanya mambo
waliyoyaamini na kuyapigania mpaka mwisho.
Hakuna sehemu yoyote ya historia
utakayosoma ukakuta kuna mtu ameibadilisha dunia au amechalenji mawazo ya taifa
kwa kufuata mkumbo.
Hapa nakuwekea baadhi ya watu
mashuhuri. Watu hawa walifanya mambo makubwa katika hii
dunia nadhani unaweza kuwatambua:
- Muhammad
- Sir
Isaac Newton
- Jesus
Christ
- Confucius
- Saint
Paul
- Christopher
Columbus
- Albert
Einstein
- Galileo
- John
Locke
- Henry
Ford
- Homer
- Alexander
the Great
- Genghis
Kahn
- Thomas
Edison
- Sigmund
Freud
- Niccolo
Machiavelli
- Charlemagne
- Adam
Smith
- Julius
Cesar
- George
Washington
Wote hawa waliweza kufanya vitu
kwa utofauti mkubwa na ndio maana mpaka leo tunawakumbuka na kuyafanyia kazi
yale waliyoyafanya.
Hivyo naomba nikushauri na wewe pia uwe wa
tofauti na hiyo ifanye iwe ndio kanuni yako ya maisha
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena