Tunaishi ili tuweze kupata
mafaniko. Mafanikio yanapatikana kwa kufanya kazi . Kazi tunazozifanya
tunahitaji kuelewa mbinu zitakazotupa mafanikio makubwa.
Hizi hapa ni mbinu saba
zitakazokusaidia kufikia mafanikio kwenye kazi zako na maisha yako yaweze kuwa
bora:
1.
Jifunze:
Jipime kama unaweza kujifunza. Jifunze kila siku. Jifunze kile unachofanya
kwenye kazi zako. Huwezi kufanikiwa kama hutojifunza. Kila siku mambo yanabadilka.
2.
Badili Tabia. Tabia
zako ziendane na kile unachokifanya. Kazi zote huwa zina kanuni. Hivyo ni
muhimu kufahamu kanuni zilizopo kwenye kazi zako. Na tabia njema siku zote
ndiyo inayoleta mafaniko bora katika maisha. Kama umekubali kufanya kazi unayoifanya
basi ni lazima ukubaliane na kanuni zake.
3.
Kuwa Na Tabia Endelevu. Tabia
endelevu ndio kipimo pekee kilicho sahihi cha kupima mafanikio. Kama umeamua
kujifunza hakikisha unajifunza kila siku. Kama umeamua kuamka mapema
hakikisha kila siku unaamka mapema. Kama una tabia njema hakikisha unaendeleza
hiyo tabia. Unapojenga muendelezo wa tabia njema kutakusaidia kufikia maisha
mazuri.
4.
Andika Hadithi Ya Maisha Yako. Fahamu
Kwamba hakuna mtu mwengine atakayefanana na wewe. Wewe ni wewe na hakuna
mtu mwengine atakayekuja kufanana na wewe. Hakuna mtu anayeweza kutengeneza
maisha yako. Kama umefanya makosa basi wewe ndiye wa kulaumiwa. Hakikisha
unatengeneza hadithi ya maisha yako. Andika kile ambacho kipo kwenye akili
yako. Ukishandika weka wazi dhamira yako kwa wengine. Baada ya hapo ishi na
dhamira yako.
5.
Achana Na Mawazo Hasi. Mpango
mzuri wa mafanikio ni kuachana na hadithi za kurudisha mafanikio yako nyuma.
Achana na stori za kukatisha tamaa. Uwezo wa mafanikio unao utakapoamua
kufanya.
6.
Fahamu Nguvu Mwendo. Fahamu
kwamba binadamu tunasukumwa na nguvu mwendo. Ukiamua kukaa bila kufanya basi
utaendelea kubaki hivyo hivyo hakuna mafanikio utakayoyapata. Ukiamua kufanya
utaendelea kufanya mpaka pale itakapotokea nguvu nyengine itakayokusimamisha
kufanya. Hivyo amua kuendelea kufanya usiruhusi nguvu ikusimamishe kwenye
mwendo kasi wa kuendelea kufanya.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena