Jumanne, 22 Novemba 2016

Chochote Unachotaka Kufanya Kwenye Maisha Yako Kinawezekana


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na kufanya chochote unachotaka kufanya kwenye maisha yako kinawezekana.

Unaweza kufanya chochote kwenye maisha yako. Na ukiamua kufanya hakuna unachoweza kushindwa. Tambua kwamba hakuna muda wa kusubiri ili uweze kuanza. Msingi wa yote hayo ni kujipangia malengo na mipango ili uweze kufanikiwa. Na mbinu sahihi ya kufanya chochote unachotaka kukifanya ili uweze kujiletea mafanikio ni kupenda kile unachotaka kukifanya na kifanye kwa furaha. Pia usiruhusu kitu chengine kiondoe furaha yako.

Hizi hapa ni njia sita (06) zitakazoweza kukufikisha kwenye safari yako ya mafanikio:

1.           Jifunze Kitu Kipya
Jinsi unavyoweza kujifunza zaidi ndivyo ambavyo unavyoweza kuongeza maarifa. Unaweza kuona vitu unavyovipenda ni vile vinavyokupatia furaha. Na vitu hivyo ndivyo vinavyoweza kukupatia furaha kwenye maisha yako.

Upo uzoefu ambao hauna mwisho. Fanya mambo mengi tofauti na usipende kujiwekea mipaka.

2.           Andika Ndoto Zako Zote
Andika kila kitu ambacho kipo kwenye ndoto zako na kile unachotaka kukifanya kwenye maisha yako. Hakikisha unachoamua kufanya kinakuletea furaha. Ukimaliza kuandaa orodha yako pangilia upya kile ambacho ni muhimu zaidi na kitu hicho kiwe cha mwanzo kukifanya.

Usiogope kuwa na ndoto ambazo zitakuchukua muda mwingi kuweza kuzikamilisha. Muda ni jambo dogo sana kama utaamua kufanya kitu ambacho unakipenda.

3.           Tengeneza Dira ya Maisha yako
Dira yako itajengwa kutokana na mawazo yako uliyonayo. Na hii ndiyo inayobeba sura mzima ya maisha yako, ndoto zako na mwelekeo wa kile unachotaka kufanya kwenye maisha yako.

4.           Tambua ni Kitu Gani Kinahitajika Ili Uweze Kufika
Ili uweze kufanya kitu chochote unachotaka ni muhimu kujuwa vitu vinavyohitajika kwa ajili ya kuweza kukufikisha huko. Kama ni mafunzo yanahitajika basi hakikisha unapata mafunzo ya kutosha. Kama ni pesa zinahitajika basi usiogope kutumia pesa ili ziweze kukupatia thamani unayoitafuta.

5.           Tengeneza Mpango Kazi Wa Miaka Mitano
Usifikirie kitu pekee cha kukufikisha pale unapotaka kwenda , lakini pia fikiria kuandaa mpango kazi wa miaka mitano  na jinsi unavyoweza kufika. Tengeneza mchanganuo ambao utakuwa na vitu vyote vya msingi. Na hiyo itakuwa ndiyo njia yako itakayokuongoza.

6.           Fanya Hatua Kwa Hatua
Kama malengo yako unayotaka kuyafanya ni makubwa ambayo yatachukuwa muda mrefu, yagawanye sehemu ndogo ndodo ili yaweze kuwa rahisi kuyatekeleza. Na njia hii itakusaidia kukutia hamasa ya kufanya zaidi na kupelekea kufikia mipango yako.

Hakikisha unajua nini unachotaka kufanya na ni muhimu kuandaa mpango kazi ambao utakufikisha na kupata chochote unachotaka kufanya. Usikate tamaa kwenye dunia hii ukiamua kufanya hakuna kinachoweza kukushinda.

Weka email yako hapa na bonyeza SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
  0784498867 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA