Jumapili, 20 Novemba 2016

Fahamu Njia Tano (05) Unazotakiwa Kuziishi Ili Watu Waweze Kukumbuka


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na njia tano unazotakiwa kiziishi ili uweze kukumbukwa kwenye maisha yako.

Kuanzia sasa ni lazima tutambue kwamba tunazo nguvu za kuacha athari chanya kwenye maisha tunayoyaishi katika dunia. Ni lazima kujitoa katika kila nafasi unayoweza kuipata. Ni muhimu kuyafanya maishi yako yawe zawadi. Siku ukitoweka duniani watu wanatakiwa waendelee kukukumbuka wewe kwa yale mazuri uliyoyafanya duniani.

Yapo makundi matano ambayo unaweza kuyafanya ili watu waendelee kukukumbuka kwa mazuri uliyofanya:

1.           Kijamii:  Yaguse Maisha Ya Wengine
Japokuwa kila mtu anakuwa na ndoto zake na matumaini katika maisha. Lakini watu wengi wanakuwa wapo tayari kusubiri na kupokea mabadiliko na ushauri wa maisha kutoka kwa wengine. Kuwa sehemu ya mchango mkubwa kwenye jamii kwa kutoa huduma ambayo itaweza kuwafikia watu wengi zaidi.

2.           Binafsi: Jiangalie Wewe Mwenyewe
Wewe ni wa pekee. Hakuna mtu ambaye atakuja kufanana na wewe. Fanya kitu ambacho ukikifanya kinaweza kuwafikia wengine.  Na kitu kizuri ambacho unaweza kukifanya na kuendelea ni kuandika. Unaweza kutengeneza blog na kuanza kuandika makala ambazo zitawafikia watu wengi au unaweza kuwa unaandika vitabu. Njia hii ya kuandika mara nyingi inawafikia watu wengi kuweza kupata maarifa ambayo yanaweza kudumu kwa muda mrefu.

3.           Kimwili: Mwili wako ndio mali kwako
Miili yetu ni thamani muhimu kwetu. Tumezaliwa tuweze kutumia maarifa yetu yote. Hakuna mtu wala jambo la kulaumu katika maisha yetu.  Miili yetu ina nguvu za kutosha kuweza kufanya kitu chochote. Tumia nguvu ulizonazo kwenye mwili wako katika kufanya mambo yaliyo bora yanayoweza kukufanya wewe uonekana shujaa wa maisha yako.

4.           Kiroho: Angalia Imani Yako
Jenga hisia ya kuiona dunia kama ina maana sana kwako. Sote tuna kitu ambacho huzifanya roho zetu zipate Amani na furaha.  Fanya unachofanya kwa uaminifu na kwa moyo wa upendo. Unapofanya kwa roho ya upendo na uaminifu unakuwa umetengeneza heshima ya kutambuliwa na kukumbukwa daima.

5.           Akili: Akili yako ndio kitovi cha udhibiti
Akili zetu ndizo zinazotuongoza nini tufanye. Mawazo yako yaweke katika kuwasaidia watu wengine kupata kile wanachokihitaji kwenye maisha yao. Thamini watu wote na ishi kwa kuwa na msaada kwa maisha ya watu wengine. Jitoe katika kuwafanya wengine wawe na maisha bora.

Hizi ndio njia tano bora za kuishi maisha yako ili watu waweze kukukumbuka. Chagua kuishi kwa kufuata njia hizi kwa ajili ya kuacha athari kwenye dunia hii.
 
Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja  kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA