Jumamosi, 19 Novemba 2016

Zijue Mbinu Za Kuendeleza Mawazo Ya Mafaniko


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mbinu za kuendeleza mawazo ya mafanikio.

Kama ungependa kuwa na mafanikio Zaidi katika maisha yako, fanyia kazi mawazo yako ili uweze kupata muongozo wa mafanikio.

Na hizi hapa ndio mbinu ninazokushauru uziendeleze kwa ajili ya mafanikio yako.

1.           Jifunze Kutafakari kwa Mtazamo Mpana
Ondoa Dhana ya kwamba haiwezekani kwenye jambo lolote unalofanya. Unapoweza kufikiria mambo makubwa na kuamini kwamba inawezekana, hapo ndipo akili yako inapoweza kuwa na mtazamo wa kuweza kufanya bila kushindwa. Kila kitu kinawezekana, ni juu yako wewe dhidi ya kufanya kwa upendo na kwa bidii ili kuweza kufikia maisha ya mafanikio. Waza mambo makubwa ambayo yatakupeleka hatua kumi mbele kufika kwenye maisha ya mafanikio. Na unapoamua kufanya usikate tamaa.

2.           Fanya Maamuzi Sasa kwa Ajili Ya Kuweza Kuishi Maisha Mazuri Baadaye
Fikiria maisha yako ya usoni. Huwezi kufanikiwa kwenye maisha yako bila ya kuwa na mtazamo wa baadaye. Lazima uishi kwa kufanya mambo ya msingi sasa ili uweze kuishi vizuri baadaye. Lazima ufikirie ni maisha ya aina gani unataka kuishi.

Mtazamo wa baadaye unaweza kukuongoza katika kufanya maamuzi yako ya kuishi maisha ya kila siku.

3.           Chukua Hatua Kwenye Wakati Mgumu
Moja ya njia mzuri ya kujenga kujiamini ni kuchukua hatua kwenye hali isiyo ya kawaida. Unapoweza kujifunza kufanya kwenye wakati mgumu unakuwa umetengeneza uwezo wako wa kuwa jasiri na kuwa na kasi ya kujenga. Chukua hatua moja kila siku ya kufanya jambo ambalo hujatarajia kulifanya. Jifunze kufanya kitu hata kama unaogopa kufanya. Fanyia kazi malengo makubwa na jenga maisha yako kwa ndoto ambazo zitakutoa kwenye hali ya kawaida.
 
Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja  kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA