Habari za leo ndugu
msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa
makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.
Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo matatu ya kujifunza
ili uweze kufikiria kama milionia.
Watu wengi wanadhani kwamba kuwa
milionia ni suala la kuja na wazo la biashara au kufanya kazi kwenye makampuni
makubwa. Wanashindwa kuelewa kwamba watu ambao wanamafanikio wanaishi kwa
kutegemea kupata pesa kama kawaida.
Njia ya kuwa huru kifedha
haitokani na kipato unachokipata bali ni ule uwezo wa kufanya na kufikiri
kuhusu pesa.
Kwenye Makala hii
nitakushirikisha mambo matatu muhimu na mawazo sahihi kuhusiana na kuweza
kuwa milionia. Kuweza kufanikisha mambo hayo sio tu kwamba ni uhakika wa
kuwa milionia, lakini ni njia za uhakika za kufanya maamuzi yalio sahihi.
1.
Jifunze Tofauti Kati Ya Mali Na
Madeni
Nadhani ninapoongelea maana ya
mali utakuwa unanielewa. Mali Inaweza kuwa vitu kama Nyumba, Uwekezaji na
Fedha zinazoweza kukuongezea thamani.
Chukulia mfano unataka kunua
gari. Gari kwa kiasi Fulani inayo thamani lakini jiulize gari ulilonunua
linakuingizia shilingi kwenye mifuko yako? Kama haiwezi kukuongezea pato lako
basi hiyo hatuwezi kuita mali bali gari hilo tunaweza kusema ni deni kwako kwa
sababu linapunguza pesa kwenye mifuko yako.
Kama gari hilo unalitumia kama
daladala au taxi basi tunaweza kuliita ni mali kwa sababu linatengeneza pesa
kila siku.
Unapoweza kufikiria kwa mtazamo
huo utagundua kwamba matumizi ya pesa yako yanatakiwa yatumike pale ambapo pesa
inaweza kuzalisha.
2.
Tambua Njia Za Kuzalisha Mapato
Watu wengi wanapatia maisha
kutokana na kufanya kazi. Kufanya kazi ni njia ya uhakika ya kuzalisha kipato.
Ni lazima ufanye kazi kila siku kama unataka kuzalisha kipato. Unaposimama
kufanya kazi basi utakuwa umesimama kutengeneza pesa.
Utajiri wako unategemea ni kiasi
gani unajituma kufanya kazi.
Kwa watu wengi kuzalisha mapato
ni suala rahisi la kufanya ambalo hufanywa kwa kuwekeza pesa. Kuwekeza kwenye
hisa ni uwekezaji mzuri kwa sababu hauhitaji uwepo wako wa moja kwa moja.
Milionia wengi wanakuwa na vyanzo mbali mbali vya kuongeza kipato.
Kumbuka uwekezaji sio lazima
uwekeze pesa. Bali pia unaweza kuwekeza muda. Kutengeneza biashara ambayo ina
uwezo wa kujiendesha wenyewe, kama tovuti, ambayo inahitaji kazi kidogo. Kazi
inapokamilika inakuwa inaendelea kwa kutumia mfumo ambao unajiendesha wenyewe.
3.
Ishi Chini Ya Njia Yako.
Haijalishi kwamba unatengeneza
kiasi cha milioni mia moja kwa mwaka au milioni moja kwa mwaka, jambo la muhimu
ni kwamba unaishi maishi ya kawaida. Usiwe kama wale watu ambao wanatumia tabia
ya asili ya kuwa na matumizi makubwa pale ambapo wanapata pesa nyingi. Kumbuka
kujenga tabia ya kutunza pesa Zaidi unavyoweza. Hata kama unapata laki moja kwa
mwezi , unaweza kuanza.
Wakati mwengine mapato yako
yanaweza kuongezeka, na hiyo ndiyo iwe njia ya kuongeza uwekezaji wako. Jaribu
kuongeza fedha inayoongezeka kwenye akiba yako, badala ya matumizi hakikisha
unaboresha maisha yako.
Hakikisha unajifunza na kufuata
njia hizi zitakazo kuvuusha kufikia milionia. Jifunze tofauti kati ya mali na
madeni, Tambua njia za kuzalisha mapato na Ishi chni ya njia yako.
Weka email yako hapa na bonyeza
NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
0784498867
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena