Jumatatu, 14 Novemba 2016

Jifunze Kutokana Na Mambo Yanayorudisha Nyuma Na Makosa Unayoyafanya


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala unayotakiwa kujifunza kutokana na mambo yanayorudisha nyuma na makosa unayoyafanya.

Jinsi tunavyoweza kumudu hali ngumu kwenye maisha ndivyo tunavyopata sura yenye kutuonesha vile tulivyo. Namna tunavyoiangalia hali ngumu inayotutokea ni jambo muhimu katika kushuhulikia makosa.

Uvumilivu na upendo ni kiungo muhimu sana katika kuyafikia mafanikio. Kuwa na sababu ni muhimu vile vile pale tunapokutana na mambo yanayorudisha nyuma. Unapoweza kukutana na makosa ni wakati mzuri wa kupata uzoefu.

Kuna msemo wa zamani unaosema kwamba mlango mmoja ukifungwa basi mwengine hufunguliwa. Kama kuna sehemu umekwama lazima kutakuwa na fursa kwenye eneo jengine. Jambo la msingi ni kuwa macho.  Kuna watu ambao wanashindwa kuona fursa hata kama mlango utakuwa wazi.

Pale mambo yanapokwenda kinyume unatakiwa kujifunza jinsi ya kubaki kwenye kufikiri kwa muda na kuendelea kubaki kwenye njia ya kutafuta ufumbuzi. Matatizo unayokutana nayo yanaweza kuwa ya muda mfupi kama utaelekeza juhudi zako katika kusonga mbele. Hakuna binaadamu ambaye hana matatizo , lakini tofauti ya kushinda na kushindwa kutatua matatizo inatokana na ile hali ya kubaki kwenye njia iliyo sahihi.  Ili uweze kushinda ni lazima ubaki njia chanya na kuwa na msukumo wa kwenda mbele.

Unapoamua kufanya lazima utarajie matatizo. Unapoamua kutatua makosa na mambo yanorudisha nyuma ni muhimu kuendelea bila ya kusimama na kukata tamaa.

Njia moja ya kuepuka makosa ni kutambua kwamba yanaweza kutokea kila siku. Jambo la msingi ni kujiandaa bila kusita. Matatizo, Makosa, Mambo yanaorudisha nyuma na kupoteza yote hayo ni sehemu ya maisha. Hayo ni mambo ambayo hatuna budi isipokuwa kukubaliana nayo. Hutakiwi kupata mshituko pale yanapokutokea.

Muhimu ni kuelewa kwamba unapofanya makosa hurudii kosa lile lile. Tambua muda gani unatakiwa kuacha na ni muda gani unatakiwa kuendelea mbele.

Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867 

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA