Jumamosi, 12 Novemba 2016

Fahamu Imani Za Pesa Zinazokufanya Ufe Maskini


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na Imani za pesa zitakazokufanya ufe maskini.

Pesa Inatenganisha Familia. Umeshaona mtu anafanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya kusaka pesa. Muda wa kukaa na familia unakuwa mdogo. Muda unapokuwa mdogo na mahusiano ya kukaa karibu na familia yanapungua.

Watu wanaweza kukulaumu kwa ajili ya kuitenga familia. Kwa sababu hii wewe unaweza kukata tamaa ya kutafuta pesa, matokeo yake unaamua kuacha kujishuhulisha sana na kubaki na njia yako ya umaskini. Ili uweze kuipata pesa ni lazima ufanye kazi sana, ni lazima ujitoe sana na ni lazima familia na watu wako wa karibu wakubali kwamba pesa ndiyo msingi wa mafanikio yenu. Badilisha Imani hii hatari na kuwa karibu na mawazo ya pesa ili uweze kufanikiwa.

Hujui Kitu. Mfumo wetu wa elimu unatuangusha sisi katika mtazamo wa pesa. Unatufundisha kuajiriwa na kupata kazi mzuri. Unashindwa kutufundisha sisi jinsi ya kupata pesa na namna ya pesa inavyofanya kazi. Unashindwa kutufundisha namna ya kuendesha biashara.

Kwa hivyo ni juu yako kujifunza yote hayo. Jifunze kutafuta pesa, jifunze kuendesha biashara na jifunze kuwa tajiri. Jiandae kwa kusoma vitabu vya pesa mara kwa mara. Unapotafuta maarifa ya pesa utaanza kubadilisha Imani yako kuhusu pesa. Mafanikio yako na utajiri yanaweza kukuwa haraka kama utakuwa na nia ya kuboresha.

Lawama. Watu ambao ni maskini wanapenda lawama zao kuwapelekea watu wengine. Wenye mafanikio wanakubaliana na lawama zao na wanakubali makosa yao, na kuchukua hatua za kuboresha makosa yao.

Kuweza kupata fedha Zaidi na mafanikio katika maisha yako, kwanza fanya uamuzi wa kutupa nje Imani hizi mbaya. Kuwa tayari kukubali Imani mpya ambazo ni mzuri kwa malengo yako. Unapoanza kujifunza mafanikio ya kupata pesa ndivyo unavyoweza kupanua uelewa wako kwa kile kinachowezekana.

Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867
 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA