Ijumaa, 11 Novemba 2016

Fahamu Imani Za Pesa Zitakazokufanya Ufe Maskini


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na Imani za pesa zitakazokufanya ufe maskini.

Katika Ulimwengu watu tunatafuta pesa kwa ajili kututumikia. Wewe ndiye bwana wa pesa na pesa ni mtumishi wako muaminifu.

Hizi hapa ni Imani mbaya kuhusu pesa na hatua za kuchukua kuondokana nazo.

Pesa si kila kitu. Baadhi ya watu wanaamini kwamba pesa haziwezi kunua furaha. Lakini fedha ni kiashiria cha mafanikio. Maskini na watu ambao hawana mafanikio wamekua na Imani hii na kuwafanya wasifanye vitu vyenye maendeleo na hivyo kupelekea kushindwa kwa upande mwengine. Watu wenye mafanikio wanakuwa na tabia zinazowaendeleza kutimiza malengo na ndoto zao.

Hujui Jinsi Ya Kupokea. Watu wengi tunashindwa kujua thamani ya kile tunachokitoa. Mfano mzuri chukulia wewe umeweza kujifunza kitu kwa miaka mitano baada ya hapo ukawa na ujuzi wa kuweza kuyafanyia kazi yale uliyojifunza. Jee unaweza kuipima thamani ya kazi unayofanya au huduma unayotoa kwa malipo unayoyapata. Jibu ni hapana kwa sababu muda uliotumia ni mwingi lakini ujira utakaopata naamini hauwezi kulipa elimu yako. Na hii ni changomoto kwa watu wengi. Kutokujua thamani na jinsi ya kupokea kunawafanya watu wafe wakiwa maskini.

Kukosa Kushukuru Kwa Kile Ulichonacho.  Anza kuwa na shukurani kwa kiasi chochote cha pesa unachokipata. Shukurani ndio mzizi wa akili, ambao unakufanya upokee na upanue mawazo yako. Na unapokuwa na shukurani uwezekanao wa kupata mafanikio unaweza kuwa mkubwa.

Una Taswira Ya Kimasikini. Unaweza kukua kama taswira yako ni ya kukua. Kama unataka kufanya tathmini kuhusu kazi unayotaka kuifanya basi wewe unatakiwa kuwa wa mwanzo kuamini kwamba unaweza. Ukijiwekea taswira hasi na Imani hasi kwamba huwezi basi wewe utakuwa mtu wa kwanza kujitengenezea sumu yako.

Mara tu unapojenga Imani unakuwa umejiletea thamani yako ambayo itakufanya ikupe nguvu za kuwa na furaha, afya njema na kuweza kuendelea kufanya vizuri katika maisha yako.

Kuweza kuleta fedha Zaidi na mafanikio katika maisha yako kwanza kabisa ni kufanya uamuzi wa kutupa nje kabisa Imani hizi mbaya. Kuwa tayari kukubali Imani mpya ambazo ni mzuri kwa malengo yako.

Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA