Jumapili, 6 Novemba 2016

Mambo Matatu (03) Ya Kuachana Nayo Kama Unataka Kudhibiti Maisha Yako


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana mambo matatu ya kuachana nayo ili uweze kudhibiti maisha yako.

Hakuna jambo zuri katika maisha kama kuishi kwa kutegemea masharti na misingi yako mwenyewe. Katika kuishi maisha yako ni muhimu kuzingatia uzibiti wa maisha yako. Kuishi kwa kuchagua njia yako ya maisha na kuishi kwa kufuata maadili yako ni jambo litakalokupa faraja kubwa katika maisha yako.

Yafuatayo ni mambo matatu unayotakiwa kuachana nayo ili uweze kudhibiti maisha yako:

1.           Achana Na Kuishi Kwa Kutegemea Maisha Ya Mtu Mwengine
Kuishi kwa kutegemea maisha ya watu wengine ni kama umekabidhi nguvu na akili yako mikononi mwa watu wengine.  Unapotegemea maisha ya watu wengine ni sawa na kuuza uhuru wako binafsi na kutapelekea kuonekana kwamba wewe huko sawa kabisa. Jitambue kwamba wewe ni wa peke yako na una uwezo wa kudhibiti maisha yako. Chagua maisha unayotaka kuishi na ishi kwa kujiamini bila ya kutegemea maisha ya mwengine.

2.           Achana Na Matarijio Yasiyokuwa Na Uhalisia
Unapojipa changamoto kunaweza kukuongezea thamani ya maisha yako na kukufanya uishi maisha yenye furaha. Achana na dhana ya matarajio. Usiruhusu akili yako ijiambie kwamba kama nitashindwa kufanya kitu hiki vizuri kwa nini najisumbua kufanya, Kama nitashindwa kujifunza kitu hiki kwa nini niendelee kufanya.

Mawazo kama hayo hayawezi kukupa udhibiti wa maisha yako badala yake yanaweza kukurudisha nyuma katika maisha yako. Ushauri wangu ni kukuomba uendelee kujaribu kufanya na kupata ujuzi mpya bila ya kujali kwamba unaweza kufanya vizuri au vibaya.

3.           Achana Na Kuanza Kujilaumu Mwenyewe Pale Mambo Yanapokwenda Vibaya
Kila mtu anafanya makosa. Na huo ndio ukweli kwamba hakuna aliye kamilika. Ili kufanya maendeleo katika maisha, lazima kuchukua hatari, Na unapofanya mambo ya hatari usiogope kushindwa. Kama unataka kuchukua udhibiti wa maisha yako na kuanza kuangalia mbele, ni muhimu kuacha kujilaumu kwa kuangalia makosa ambayo umewahi kuyafanya nyuma. Jiulize ni kipi cha kujifunza kutoka kwenye mambo yaliyopita na fanya juhudi ya kuangalia kufanya vizuri zaidi baadaye.

Sio jambo rahisi kudhibiti maisha yako na ndio maana walio wengi wanashindwa njiani, lakini kuchukua hatua na kuanza njia mpya ya maisha ni thamani kubwa katika kuboresha maisha yako. Hivyo kuanzia leo achana na maisha tegemezi na ishi maisha yako, Achana na matarajio yasio na ukweli na achana na kuanza kujilaumu wewe mwenyewe kwa makosa yako unayoyafanya. Chukua hatua leo ili maisha yako yawe na mafanikio.

Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.

Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
            ali76khamis@yahoo.com
            0784498867 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA