Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo matatu ya kujifunza
ili uweze kuishi maisha bora.
1.
Jifunze Kutokana Na Hali
Unayopitia
Maisha unayopitia usifikirie
kwamba hakuna njia nyengine ya kukutoa hapo ulipo. Hali yoyote unayopitia ya
maisha inaweza kuleta mafanikio. Hivyo jifunze kutokana na hali yoyote
unayoweza kukukabili. Na usifikirie kwamba siku zote utapata matokeo mazuri
katika maisha yako, bali hali inapokuja kinyume ichukulie kama somo la
kujifunza katika maisha yako.
2.
Kuwa Bora Kuliko wote
Usiishi kwa kujisikia vibaya kwa
kujilinganisha wewe na wengine, kila mtu ni wa kipekee na ni muhimu kufanya
vizuri kuliko watu wengine.
3.
Kila Tatizo Lina Suluhisho
Unapopata tatizo ni muhimu
kulitatua haraka, Unapoweza kutatua tatizo kwa haraka ndivyo utakavyojisikia
Amani.
Muhimu; Jifunze
kutokana na hali unayopitia, Kuwa bora kuliko wote na tambua kwamba kila tatizo
lina suluhisho.
Weka email yako hapa na bonyeza
Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
0784498867
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena