Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na Mafanikio unayoweza
kuyapata kwa kuanzia na hali uliyonayo sasa.
Mara nyingi tunawaangalia watu
waliofanikiwa na kuona kama wana bahati. Ukweli ni kwamba watu waliofanikiwa
wanatumia juhudi na maarifa kuweza kuleta mafanikio. Kuna mambo mengi ya msingi
ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwa wanamafanikio waliofanya vizuri duniani.
Uchaguzi wa kuishi maisha
unayoyataka yako ndani ya uwezo wako. Unaweza kuendelea kuchagua vitu vibaya
viendelee kuumiza kichwa chako ama kufanya mambo mazuri yatakayobadili maisha
yako.
Uamuzi Ni Ufunguo Wa Maisha
Yako. Uamuzi ni kitu ambacho kipo ndani ya uwezo
wako lakini mara nyengine tunaona mambo ni magumu na kushindwa kubaki kwenye
maamuzi mazito unayotaka kufanya kwa sababu tumezoea kufanya kwa kutegemea
mteremko. Lakini kama una lengo na ndoto ni muhimu kufurahia hatua ndogo za
mafanikio unayoyapata. Endelea kusonga mbele hata kama hujusikii kufanya hivyo.
Uamuzi ndio nguvu yako ya kuyafikia malengo yako katika maisha.
Wasaidie Wengine Kuwa Na Maisha
Mazuri. Unapoweza kuboresha ustawi na furaha kwa
watu wengine ni sababu muhimu ya wewe kupata furaha pia. Zingatia kwamba upendo
na msaada unaanzia nyumbani kwako kwanza, marafiki , majiranii na jamii kwa
ujumla. Ni muhimu kutenga muda wako kwa ajili kusaidia mahitaji ya wengine, na
hii itawafanya watu wajisikie bora na kukufanya wewe kuwa na mafanikio.
Kumbuka mafanikio ni kile
ulichoweza kufanya bila kujali umeanzia wapi. Anza sasa popote pale ulipo. Amua
na Ishi kwa kuwasaidia wengine kupata kile wanachotaka.
Weka email yako hapa na bonyeza
Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
0784498867
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena