Jumatano, 9 Novemba 2016

Tengeneza Taswira Ya Mtazamo Chanya Kwa Ajili Ya Maandalizi Bora Ya Maisha Yako


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na kutengeneza taswira ya mtazamo chanya kwa ajili ya maandalizi ya maisha bora.

Moja ya mambo muhimu ambayo yanaweza kukupa fursa ya mafanikio yako na furaha ni jinsi gani unaweza kuona taswira ya kivuli chako. Ukiwa na taswira chanya ni rahisi kuwa na nguvu ya kukabiliana na changamoto za maisha. Hata kama mambo yatakuwa magumu unajua kwamba unaweka maslahi na thamani yako kwanza katika mambo ambayo yanakuwa na mtazamo chanya  katika moyo wako. Kuwa na taswira ya mtazamo chanya kutakujengea sifa kwa watu wako wa karibu na pia unakuwa umejitengenezea njia ya kushi maisha bora.

Kuwa Na Ujasiri Wa Kusimama Na Maamuzi Yako Mwenyewe
Unapokuwa na picha yenye taswira ya mtazamo chanya kwenye akili yako, utakuwa umeweza kusimamia maamuzi yako. Jiamini wewe mwenyewe na kuwa na Imani katika uwezo wako ulionao na fanya maamuzi mazuri. Hali hiyo itakujenga katika kusimamia kitu ambacho unafikiri kwako ni sahihi kufanya.

Wakati unapoamua kufanya maamuzi iwe ni kwenye kazi, nyumbani au kwenye mahusiano yako na kama taswira ya mtazamo wako iko imara unaweza kujisikia salama zaidi na kupata matumaini katika maisha yako. Na hii inaweza kukupa nguvu na ujasiri wa kufanya kazi kwa bidii. Vile vile hii italeta ndoto zako kuwa za kweli.

Ukiweza kuishi kwa kufuata taswira halisi ya muonekano wako kuna uwezekano mkubwa wa kuishi kwa kufuata maadili na malengo , ambayo ni msingi mkubwa kwa ridhaa ya baadaye na kuridhika na maisha.

Ukiwa na Mtazamo Chanya Hutoweza Kuhofia Kushindwa
Kama utaweza kuwa na fikra za mtazamo chanya si rahisi kuwa na hisia za hofu kwenye kushindwa. Ukiweza kuwa na nguvu za mtazamo chanya ni rahisi kushinda.

Ishi kwa kuwa na mtazamo chanya na kuwa jasiri wa kusimamia maamuzi yako.

Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
0784498867 

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA