Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana Njia sahihi za kupanga muda
kwa mafanikio ya maisha yako.
Watu waliopata mafanikio makubwa
ni watu ambao wanajituma katika kuyasaka mafanikio. Waliopata mafanikio hawakupata
kwa bahati mbaya, bali walifanya maandalizi ya kutosha, walipanga mipango yao
vizuri na waliweza kuupangilia muda wao vizuri kwa kufanya yale mambo ambayo
yana umuhimu kwao.
Hizi hapa ndio njia ambazo watu
waliofanikiwa wanazitumia katika kupanga muda wao vizuri:
1.
Wanahifadhi Maamuizi Yao Katika
Kufanya Mambo Muhimu.
Mara nyingi tunapata kuona watu
wenye mafanikio ni watu ambao wanarahisisha mambo yao. Ni watu ambao
wanapunguza kufanya maamuzi kwenye mambo yasiyo ya muhimu kwao. Watu hawa
hawana muda wa kupoteza wa kufikiria kwamba watakula nini au watavaa nini. Ni
watu wanaofanya mambo yao kwa muda walioupanga. Wanafahamu uwezo wao na
kukazana katika kufanya maamuzi ambayo yatakuwa na athari katika maisha yao.
2.
Wanaendesha Mambo Yao Kwa
Kufuata Ratiba Ya Asubuhi.
Ili uweze kupanga muda wako wa
siku vizuri, ni lazima siku yako uianze asubuhi. Watu walioweza kuleta
mafanikio kwenye maisha yao wanaianza siku kwa Kusoma, Kufanya Mazoezi, Kufanya
Tahajudi, Kuweka kipaumbele mambo ambayo ni muhimu kwa mafanikio ya maisha yao.
Wanahakikisha mambo yote muhimu ya siku wanayaanza kuyafanya asubuhi. Watu
waliofanikiwa wanatengeneza ratiba maalumu ambayo huweza kuifanyia kazi kila
siku asubuhi wanapoamka.
3.
Wanafanya Maandalizi Ya Mipango
Yao Usiku.
Kumbuka kabla hujafanya kitu
chochote maandalizi ndio msingi wa mafanikio yako. Usisisubiri mpaka siku
iingie ndio ufanye maandalizi. Ni muhimu kupanga siku usiku kabla ya siku
husika. Ukipanga siku usiku, unapoamka utaona kila kitu kinakwenda vizuri.
4.
Wanapanga Mipango Ya Baadaye.
Moja ya tofauti kubwa kati ya
watu wenye mafanikio na ambao hawana ni kwamba wenye mafanikio wanafikiria kwa
kina kuhusiana na mawazo na mipango wanayotaka kufanya. Hii inawafanya kufanya
maamuzi sahihi.
5.
Wanaweka Kipaombele.
Watu waliofanikiwa wanatambua
kwamba kama hawajaweka kipaombele kwenye mambo wanayoyafanya ni rahisi kufanya
mambo ambayo hayako kwenye malengo. Vipaombele ndivyo vinavyowafanya waweze
kutumia muda wao vizuri na kuweza kufanya mambo ambayo ni ya lazima.
Weka email yako hapa na bonyeza
Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena