Jumatatu, 24 Oktoba 2016

Fahamu Maana Halisi Ya Pesa

 
Linapokuja suala la ufahamu wa pesa, watu wengi wanashindwa kujua maana halisi ya pesa.

Changamoto iliyopo kuhusu pesa ni kwamba, wakati kila mtu anahitaji kupata pesa za kutosha za kuweza kutimiza ndoto yake. Lakini hata unapoweza kuzipata pesa za kutosha utaona bado pesa hazitoshi kukidhi mahitaji yake na kutimiza ndoto alizojiwekea. Pesa itaweza kutosha pale utakapoweza kuiangalia kwa mtazamo tofauti.

Ni muhimu kutambua kwamba pesa inahitaji mazingira mazuri ili iweze kustawi.

1.           Pesa Huweza Kufanya Mambo Kuwa Mazuri 
Unapokuwa na pesa ni lazima uifanyie matumizi. Lazima ufikirie njia ya kuweza kuizalisha. Waswahili wana msemo wanasema pesa ni sabuni ya roho. Pesa haiwezi kuwa na thamani kama itabaki sehemu moja kwa muda mrefu. Fedha inapenda kuona mambo mapya. Inapenda kuona inafanyiwa uwekezaji. Unapoweza kuiwekeza pesa ndivyo unavyoweza kuiongezea thamani yake.

2.           Pesa Inahitaji Kuiwekea Lengo maalumu 
Umeshawahi kugundua kwamba, kama kuna mahitaji unataka kununua, basi kwa mahitaji hayo utaona pesa inaonekana. Lakini kama umejiwekea malengo maalumu kwa ajili ya pesa hiyo, utaona pesa inakuwa ngumu kuipata. Hivyo tambua kwamba kama huna lengo maalumu kwenye akili yako ni rahisi pesa kupotea. Na hii inapotea kwa sababu ni rahisi kufanya matumizi yasiyo ya msingi. Matumizi mbayo hujayawekea malengo ni sawa na kupoteza pesa ulioyoitafuta kwa muda mrefu.

3.           Pesa Inahitaji Malengo Ya Muda Mrefu 
Hili ni jambo muhimu ambalo mara nyingi wanauchumi wanalizungumzia.  Pesa ni lazima iwekewe mipango ya muda mrefu. Moja ya sababu ambayo inatufanya tunakuwa na matumizi ya pesa ni kutokana na kufanya matumizi tunapozipata pesa. Huwa tunapenda kufikiria matumizi ya muda huo huo. Kufanya hivyo kunaathiri kutoyafikia malengo ya muda mrefu.

4.           Pesa Zinapenda Kumfuata Mtu Anayezipenda 
Moja ya sifa kuu ya pesa ni kwamba huwa zinakuwa na tabia ya kukimbilia kwa mtu anayezipenda. Kama utashindwa kutambua matumizi sahihi ya pesa, basi fahamu kwamba zitamfuata mtu mwenye kujua thamani ya pesa.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA