Jumanne, 25 Oktoba 2016

Zifahamu Changamoto Tano (05) Zinazoweza Kukupatia Mafanikio Makubwa Kwenye Maisha Yako


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania.

Ni mara nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina Imani kwamba utakuwa unapata maarifa ya kutosha. Leo hii nimefanikiwa kukeletea Makala inayohusu changamoto zinazoweza kukupatia mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

Katika maisha watu wengi  hawapendi  kujihusisha na mambo ambayo yanawapa changamoto. Yapo mambo ambayo binaadamu mara nyingi tunakuwa wazito kuyafanya. Tunashindwa kuyafanya kwa sababu ya kuhofia usumbufu unaoweza kujitokeza. Uvivu unachangia kwa asilima kubwa kushindwa kufanya mambo ambayo yanaweza kuleta mafanikio. Ukweli ni kwamba mambo yanayotupa changamoto kwenye akili zetu tukiweza kuyafanya ndiyo yanayo tuwezesha kufikia mafanikio makubwa.

Hizi hapa ndio changamoto ambazo ukiweza kuzitatua zinaweza kukupatia mafanikio makubwa:

1.           Fanya Mambo Yaliyoshindikana
Ni kawaida kwa binaadamu kufanya mambo ambayo ni rahisi kuyafanya. Binaadamu huwa hatupendi usumbufu. Unapoweza kufanya mambo magumu yaliyoshindikana sio tu yanaweza kukuletea changamoto lakini pia yataweza kukupeleka kufikia kwenye mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

2.           Amka Mapema
Kuamka mapema unaweza kuiona kama ni changamoto rahisi, lakini watu wengi tunakuwa wavivu wa kishindwa kuamka mapema. Unapoweza kuamka mapema asubuhi itakusaidia kupata muda wa kutosha kuweza kukamilisha kazi zako kwa wakati. Kuamka mapema kutakufanya uweze kutengeneza mpango wa siku yako mzima, kuamka mapema kutakuwezesha kufanya mazoezi, tahajudi na kuweza kuiweka akili sawa.

3.           Ongea Mbele za Watu
Changamoto kubwa inayowasumbua watu wengi ni kushindwa kuongea mbele za watu. Kuweza kuongea mbele za watu kunajenga uwezo wa kujiamini. Ili iwe rahisi kwako kuongea mbele za watu ni muhimu kuchagua mada unayoifahamu na ambayo unaipenda.

4.           Sema Hapana
Unatakiwa kusema hapana kwenye yale mambo ambayo hayana faida kwenye mipango yako. Unapoweza kusema hapana utaruhusu kupata muda wa kutosha wa kufanya yale mambo ambayo yana ulazima kwako. Hakikisha unatumia neno hapana kwenye mambo ambayo hayana msingi wowote kwako.

5.           Usiahirishe mambo
Usipende kuwa na tabia ya kuahirisha mambo. Kama kuna mambo ambayo ni muhimu kuyafanya hakikisha unafanya na kuweza kukamilisha kwa muda muafaka. Usipende kuwa na tabia ya mazoeya ya kusema nitafanya kesho  kama unataka kuongeza thamani ya maisha yako.  Ni muhimu kuzingatia muda kwa kila jambo ulilopanga kulifanya na hakikisha unalikamilisha.

Ili uweze kuboresha maisha yako ni muhimu kuzingatia changamoto hizo. Fanya mambo yaliyoshindikana, hakikisha unaweza kuamka mapema, ongea mbele za watu, jifunze kusema hapana na mwisho acha tabia ya kuahirisha mambo.

Najua mambo haya yanaweza kukupatia usumbufu kwa sababu umeamua kuanza tabia mpya ambayo hujaizoeya. Lakini pia nakushauri usipende kufanya mambo kwa mazoeya.
Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA