Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na ishara zenye kuonesha
mwanga wa mafaniko wa maisha yako.
Katika maisha ni jambo la rahisi
kuona kwamba umeshindwa. Ni kawaida kwa mtu kuweza kuwa na hisia ya kushindwa.
Kuna wakati unatokea tunapuuzia vitu vidogo. Unapojiona wewe kwamba hujafikia
utajiri wa kuitwa milionia au huna gari zuri tayari unajenga hisia kwamba
umeshashindwa, lakini ukweli ni kuwa mtazamo wako wa hisia hauko sahihi.
Fahamu kwamba katika maisha ya
mafanikio zipo alama nyingi ambazo zinaweza kukuonesha mafanikio yako katika
maisha.
Na hizi hapa ni ishara saba
zinazokuonesha kwamba unaendelea kufanikiwa katika maisha:
1.
Umeweza Kupandisha Viwango
Vyako.
Jambo lolote unalolifanya kwa
sasa unalifanya kwa kuzingatia viwango vyenye ubora wa hali ya juu. Kwa sasa
huwezi kuvumilia uovu wa watu wengine na wewe pia hufanyi maovu. Kama wewe
unaongoza watu basi uongozi wako unawafanya watu waweze kuwajibika kwa vitendo
kwenye kazi zao.
2.
Umeweza Kujifunza Kwamba
Vipingamizi na Kushindwa ni Sehemu ya Ukuaji Wako.
Hakuna mtu aliyeweza kupata
mafanikio asilimia mia moja pasipo kuwa na vipingamizi. Maisha ni kupata na
kukosa. Hivyo ishi kwa kutambua kwamba vikwazo ni ishara ya kufanya vizuri.
Uhalisia unaonesha kwamba hakuna kitu ambacho kinaweza kukurudisha nyuma kama
umeamua kukua. Ukiweza kufikia kiwango hicho basi hiyo ndiyo ishara ya safari
yako ya ushindi.
3.
Umeweza Kutengeneza Mfumo Wa
Watu Ambao Wako Tayari Kukupa Msaada Wa Jambo Lolote.
Kama umeweza kutengeneza watu
nyuma yako ambao wako tayari kukuona wewe unapiga hatua kwenye maisha yako.
Watu hao wako tayari kwa hali na mali kuona maisha yako yanakamilisha ndoto
zako, basi tambua kwamba hiyo ni ishara ya mafanikio.
4.
Wewe Sio Mtu Wa kulalamika.
Kwa sababu unajua kweli hakuna
kitu kinachoweza kukufanya ulalamike. Kama wewe umeanza kuwa huna tabia ya
kulalamika basi ujue kwamba hiyo ni ishara moja wapo ya mafanikio yako. Watu
waliofanikiwa hawalalamiki na wanaishi maisha ya amani.
5.
Unayo Mambo Yanayokufanya
Uangalie Mbele.
Kama huna kitu ambacho
kinaonesha kwamba unasonga mbele kwenye maisha yako basi unajiua wewe mwenyewe
pole pole. Watu waliofanikiwa wanatengeneza mipango na malengo inayowafanya
wafikirie mbele. Siku zote wanafikiria mambo ambayo yanawasukuma kwenda
mbele kimaisha.
6.
Hujali Watu Wanavyo Kufikiria.
Unatambua kwamba huwezi
kumfurahisha kila mtu. Unakuwa na ufahamu kwamba watu wanavyokuwa na mtazamo na
mawazo tofauti kwa wengine hayana mashiko. Ukweli wako unaujua mwenyewe na
hakuna mtu mwengine anayeweza kujua kuhusu wewe.
7.
Wewe Ni Mtu Wa Furaha.
Furaha ndio maana halisi ya
mafanikio. Haijalishi una kiasi gani cha pesa kwenye akaunti yako, una nyumba
kubwa au gari la kifahari. Kama wewe ni mtu wa furaha basi hiyo ndiyo funguo ya
mafanikio yako.
Ili uweze kufanikiwa kwenye
maisha yako ni muhimu kuzingatia Ishara hizo. Pandisha viwango vyako vya
maisha, jifunze vipingamizi na kushindwa kama sehemu ya ukuaji wako, tengeneza
mfumo wa watu walio tayari kuwa nyuma yako, usiwe mtu wa kulalamika, Kuwa na
mambo ya kuangalia mbele, usijali watu wanavyokufikiria na mwisho ishi kwa
furaha daima.
Weka email yako hapa na bonyeza
NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena