Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na kuweka mipango mizuri
katika kipindi cha miaka mitano ijayo ili uweze kufika safari yako ya
mafanikio.
Miaka mitano inaweza kuonekana
kama muda mrefu kama umeweka mipango na unajua nini unataka kufikia.
lakini bila mipango , miaka mitano inaweza kupita haraka sana.
Hizi hapa ndio hatua tano ambazo
ukizifuata zitakusaidia kuwa na uhakika wa kuishi maisha bora baadaye:
1.
Amua Ni Nini Unataka Ufikie
Ndani Ya Kipindi Cha Miaka Mitano Ijayo.
Amua nini unataka kupangilia
ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo. Amua kama unataka kuanzisha biashara
yako mwenyewe.
Mipango ni sehemu muhimu kwa
kuhakikisha unapata kile unachotaka. Maisha yamejawa na matukio mengi ya
uwezekano, hivyo lazima ufanye kazi kwa bidii ili kufikia kile unachotaka ndani
ya kipindi cha miaka mitano.
Chukua kalamu na karatasi na
andika majibu ya maswali haya: Jee ni nini unataka kufikia? Ni muda gani lengo
lako itachukua kulifikia? Kitu cha kwanza nahitaji kufanya nini?
2.
Tathmini Malengo Yako Kila Mwezi.
Kama uliweka lengo lako wiki
iliyopita au miaka mitano iliyopita ni muhimu kufanya tathmini ya mara kwa mara
malengo yako. Maisha yako yanaweza kuwa yamebadilika au vipaumbele vingine
huenda vimeibuka, hivyo hakikisha unazingatia mambo ya muhimu kwako katika
kufanya tathmini ya kila mwezi. Kwa mfano umepanga kunua nyumba eneo fulani
lakini mara ukabadilisha mawazo kutokana na mabadiliko yaliyotokea. Hivyo kaa
chini mara moja kwa mwezi na andika majibu ya maswali haya: Jee lengo hili bado
ni muhimu kwangu? Jee bado nina shauku ya kutaka kutekeleza wazo langu?
3.
Pitia Malengo Yako Kila Siku.
Watu wengi wana malengo, lakini
watu waliofanikiwa zaidi huweka akili zao mbele kwenye malengo yao wakati wote.
Ni muhimu kugawa malengo makubwa katika malengo madogo madogo. Hii itakusaidia
kuhakikisha kila siku unafanya kitu kwenye malengo yako.
Jiulize kila siku: Ni vipi
naendelea na malengo yangu? Ni kazi zipi naweza kufanya kwa siku ili kuweza
kuwa karibu na lengo langu? Nifanye nini leo ili niweze kufikia malengo yangu
ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo? Jee naweza kufikia malengo yangu
mapema zaidi?
4.
Weka Ahadi Kila Wiki Kwa Malengo
Yako.
Unapomaliza kuandaa malengo
yako, kilichobaki ni muda wa kutekeleza. Tambua kwamba malengo yako unaweza
kuyafikia kwa urahisi iwapo utaweza kuanza kazi mara moja. Leo ni wakati bora
wa kuanza kuliko kusubiri kesho.
Mwanzoni mwa kila wiki, andika
yale unayodhamiria kuyafanya kwa wiki hiyo, na hii ni kwa ajili ya kuelekea
kufanikisha lengo lako. Sio lazima ufanye kitu kikubwa kila wiki, hata kufanya
kitu kidogo kutakusaidia kuona kwamba unaweza kuelekea lengo lako la kila siku.
5.
Andika Matokeo Yote
Yanayowezekana.
Chukua kalamu na karatasi na
andika mambo yote ambayo unaweza kuyafanya ili uweze kukamilisha malengo yako.
Wakati mwengine kutakuwa na changamoto za kutisha, lakini hiyo ndio njia nzuri
kwako ya kutatua matatizo ya kuelekea safari yako.
Angalia njia za kufanya kwa
ajili ya kuboresha kwa kila lengo, na mara kwa mara angalia majibu yako.
Huenda ukashindwa kudhibiti siku
zijazo, lakini unaweza kudhibiti hali ya kukabiliana na maisha kutokana na njia
uliyoichagua. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo unaweza kukabiliana na
changamoto na matatizo mbali mbali, lakini watu waliofanikiwa zaidi waliweza
kukabiliana na hali hiyo kwa kutatua changamoto zao. Na mwisho waliweza
kufika kilele cha safari yao ya mafanikio.
Weka email yako hapa na bonyeza
SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena