Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na makosa makubwa
wanayoyafanya watu wanaoshindwa kufikia mafanikio.
Katika ulimwengu wa sasa kila
mwanaadamu anaishi kwa kutamani kuyafikia mafanikio. Kwenye mafanikio
kuna kupata na kukosa. Huwezi kufanikiwa pasipo na kutenda makosa, lakini
makosa hayo ndio ngao kuu ya wanaadamu kufikia mafanikio kama watazingatia
kanuni, ushauri na misingi sahihi ya maisha.
Haya hapa ndio makosa makubwa
matatu ambayo watu wanashindwa kufikia mafanikio yao kama wataendelea
kuyafanya:
1.
Kujiwekea Mipaka.
Ni kosa kubwa kujiwekea mipaka
kwa jambo lolote lile. Badala yake ishi kwa kuwa na ndoto ya kupata zaidi ili
mafanikio yako yawe makubwa zaidi. Kuwa na mipaka inaweza kuwa ndio chanzo cha
majaribio mengi ya kushindwa katika mafanikio. Mipaka inaweza kutupa imani
dhaifu kwamba hatuwezi kuyafikia mafanikio. Unapoamua kufanya bila ya mipaka
utaweza kujenga misingi ambayo inaweza kukuongoza katika njia ya mafanikio.
Usitumie vikwazo ambavyo
vinatokana na mipaka uliyojiwekea kama ndio njia moja wapo ya kukata tamaa. Ni
jambo jema kutambua kwamba kwenye maisha hakuna kinachoshindikana.
2.
Hawajifunzi Kutokana Na Makosa
Wanayoyafanya.
Katika maisha makosa hayawezi
kuepukika. Mara nyingi makosa huwa yanawarudisha watu nyuma. Jifunze kwa kila
kosa unalolifanya na ukifanya hivyo unakuwa umetengeneza njia yako ya
mafanikio.
Unaweza kufanya makosa zaidi ya
elfu moja lakini kama hurudii makosa unayofanya basi utakuwa umeweza kujifunza
na umeweza kufanikiwa kukua. Watu waliofanikiwa hawafanyi kosa hili.
3.
Hawana Hamasa.
Hamasa ndio inayowasukuma watu
kwenye mafanikio. Huwezi kufanikiwa katika kitu chochote kile bila ya kuwa na
hamasa. Fanya bidii yako ya hali ya juu ili uweze kupata kile unachotaka.
Tafuta vitu vinavyoweza kukupa hamasa zaidi kwenye lile eneo unalolifanya.
Hamasa huibua nguvu ya kufanikisha lengo lolote la maisha. Hamasa inajenga
ukomavu wa muendelezo wa kitu mpaka pale kinapotokea na kuwa uhalisia.
Ili uweze kupata mafanikio ya
kweli katika maisha usirudie makosa hayo. Hakikisha hujiwekei mipaka kwa jambo
lolote unalolifanya. Hakikisha unajifunza kwa kila kosa unalolifanya na mwisho
lazima uwe na hamasa kwa kitu chochote ulichoamua kufanya. Ukiweza kutekeleza
haya kwa muda mfupi unaweza kuyaona matunda ya mafanikio ya maisha yako.
Weka email yako hapa na bonyeza
SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena