Jumamosi, 29 Oktoba 2016

Yajue Mambo Matano (05) Kutoka Kwa Wafanyabiashara Wenye Mafanikio


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo matano muhimu kutoka kwa wafanyabiashara wenye mafanikio.

Watu wengi ambao ni wafanyakazi huwa wana mawazo na shauku ya kutaka kuanzisha biashara. Na changamoto kubwa ni kuwa hawajui waanzie wapi ili waweze kufanikiwa katika biashara watakazozianzisha. Unapoamua kuanzisha biashara unahitaji kujitoa kweli, na lazima uweke mipango mizuri.

Uamuzi wa kuianzisha biashara ni wa busara lakini ni vyema kujua mbinu bora zitakazoweza kufanikisha biashara hizo. Kama umeamua kuingia kwenye biashara ni vizuri kujifunza na kusikiliza ushauri kutoka kwa wafanyabiashara wenye ufanisi mkubwa wa biashara unayotaka kwenda kuifanya.

Na huu hapa ndio ushauri mzuri kutoka kwa wafanyabiashara waliofanikiwa kwenye biashara zao:

1.           Tumia Hekima Wakati Wa Kuchagua Washiriki
Mtandao wa watu unaweza kuwa na mchango mkubwa kwenye biashara yako. Chagua marafiki watakaoweza kukusaidia kufanya vizuri katika biashara yako . Watu waliokuzunguka wana mchango mkubwa katika biashara unayoifanya. Hakikisha watu uliowachagua wanakuwa ni watu wenye malengo mazuri katika maisha yao.

2.           Kuwa Na Wawakilishi
Watu ambao wanatumia muda wao katika kuweka juhudi zao kwenye kujenga biashara huwa wanakuwa wazito sana linapokuja jambo la majukumu na kuwapa watu wengine. Ni vyema kwenye biashara yako uwe na wajumbe watakaokusaidia katika kazi zako. Huwezi kufanya kila kitu wewe mwenyewe. Kufanya kila kitu wewe utajipa mzigo mkubwa ambao unaweza kushindwa njiani.

3.           Usiruhusu Kushindwa
Haijalishi unapitia magumu kiasi gani, lakini lazima kutakuwa na njia nyepesi. Unapoona umeshindwa njia moja, buni njia nyengine itakayoweza kufanya vizuri. Hata hivyo wajasiriamali wakubwa duniani wanaamini kwamba hakuna linalishindikana kama umeamua kufanya jambo kubwa.

4.           Wajue Wateja Wako Vizuri
Ni muhimu kuwajua wateja wako kwenye biashara unayofanya. Biashara inajengwa na misingi ya kuweka akili na mawazo yako katika kuwajua wateja wako. Wateja ndio watakaokufanya uweze kukua kwenye biashara yako. Hivyo unapoamua kutengeneza bidhaa zingatia mahitaji ya wateja wako.

5.           Usitosheke Na Ulipofikia
Siku zote jifunze mambo yanayohusiana na biashra yako. Usipime mafanikio yako ya biashara kwa kuridhika na kiwango ulichofikia. Hakikisha kila siku unaongeza thamani ya biashara yako. Wafanyabiashara wenye mafanikio wamekuwa na mafaniko kwa sababu waliweza kuzikuza biashara zao.

Ndugu msomaji wa makala hii nakushauri uzingatie haya mambo matano kama kweli umeamua kufanikiwa kwenye biashara uliyoanzisha.

Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required
    

Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA