Jumamosi, 29 Oktoba 2016

Jifunze Majibu Ya Maswali Manne (04) Yanayoweza Kukupatia Utabiri Wa Mafanikio Katika Maisha Yako


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na utabiri wa mafanikio wa maisha yako.

Tunapozungumzia mafanikio ya maisha yapo mambo muhimu unayotakiwa kuyatimiza. Na sio tu kuwa na pesa za kutosha lakini ni pamoja na kuwa na afya njema, kuwa na mahusiano mazuri na watu pamoja na familia, kutimiza malengo yako na mambo mengine mengi ambayo yanatufanya tuishi maisha tunayoyataka.

Haya hapa ndio maswali manne ambayo yanatabiri mafanikio ya maisha yako.

1.           Je, Wewe Tayari Umejiandaa Kiakili?
Watu wenye mawazo ya ukuaji kwenye akili zao huona kushindwa kama ndio somo la uhakika ambalo linaweza kumtoa kwenye kifungo cha umaskini na kumpeleka kwenye mafanikio.

Ni kawaida kwake kukubaliana na changamoto, kuboresha misingi mbali mbali ya maisha yake ili aweze kufikia malengo aliyojiwekea.

2.           Una Furaha?
Mtazamo chanya ni kiungo muhimu kwa mafanikio na kukusaidia kukuweka katika hali ya furaha na kuweza kuwa na matumaini mazuri. Kufurahia kila hatua unayoipiga kwenye maisha yako kutakuongezea nguvu ya kuweza kupambana zaidi katika kuyafikia malengo yako makubwa. Ili uweze kuwa na furaha lazima uwe na upendo na mahusiano mazuri kwa watu.

3.           Je, Una Mapenzi Na Unachokifanya?
Moja ya sababu muhimu ya kufanikiwa kile ulichoamua kufanya ni kufanya kwa mapenzi ya hali ya juu. Hakikisha unapata nguvu na msukumo wa kutaka kuendelea kufanya. Kila siku weka uhakika wa kuboresha hatua nyengine zaidi.

Kama huna mapenzi na unachofanya ni bora kuacha kufanya, kwa sababu ukiendelea kufanya ni kama unapoteza muda wako. Ishi kwa kufanya yale mambo unayoyapenda.

4.           Uko Tayari Na Kukabiliana Na Hatari Ya Kupoteza?
Watu ambao wamepanga malengo yao ya kupata mafanikio tayari wanajua lazima watakumbana na hatari. Tayari wameshaweka maandalizi ya kukabiliana na hatari hizo zinapojitokeza. Hivyo hakuna kitu ambacho kitawafanya wawe na msongo wa mawazo kwao.

Kumbuka kwamba huwezi kuwa na mafanikio makubwa kama utakuwa hujaweza kutimiza mahitaji yako ya lazima. Mahitaji ya lazima ni kama chakula, mavazi na malazi. Kama umeweza kukamilisha hayo ndio sasa unakwenda kwenye hatua nyengine ya mafanikio makubwa. Mafanikio hayo yatapatikana kutokana na malengo na mipango imara uliyojiwekea pamoja na kufuata utabiri unaokuongoza kuelekea kwenye safari ya mafanikio ya maisha yako.
 
Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA