Katika dunia tunayoishi kila mtu
anapenda maisha ya furaha. Watu wanapopata misokosuko ya maisha sio kwa sababu
hawataki wafanikiwe.Watu wote wanataka mafanikio. Wanataka waishi maisha yaliyo
sawa na bora. Lakini watu wanafika mahala ambapo wanakumbana na changamoto za
maisha. Hali inayopelekea kushindwa kujuwa ni hatua zipi wachukuwe.
Lengo la makala hii ni
kukushirikisha ndugu msomaji changamoto hizi tatu wanazokutana nazo watu kila
siku. Vile vile utajifunza njia bora za kufanya ili kutatua changamoto
hizo. Njia hizi zitakusaidia wewe kutatua changamoto hizi na kuweza kuishi
maisha ya amani. Maisha ya furaha na afya njema kwenye maisha
yako yote.
1.
Sina Muda: Watu
wengi wanapenda kusema wamekosa muda wa kufanya. Sina muda wa kufanya kazi
vizuri. Sina muda wa kukaa karibu na familia. Sina muda wa kufanya chochote ili
niweze kupata mafanikio. Wamekosa muda wa kufurahia maisha. Ukisema huna muda
wa kufanya utakuwa unakosea. Muda unao wa kutosha. Lakini tatizo ulilonalo hapa
ni kwamba umeshindwa “ Kuupangilia Muda” wako vizuri.
Hizi hapa ni baadhi ya mbinu za
kufanya ili uweze kuongeza thamani ya kupangilia muda vizuri:- Jifunze
kusema hapana. Unaposema hapana kwenye vitu vingi
ambavyo havina thamani kwako kutakusaidia kujiweka huru na matumizi mabaya
ya muda. Kusema hapana kutakusaidia kufanya yale mambo ya msingi ambayo
unatakiwa kuyafanya na utaepukana na mambo ambayo hayana ulazima
kuyafanya.
- Huhitaji
muda mwingi ili kazi ifanyike. Watu wengi
waliofanikiwa wanatumia kati ya dakika 30 hadi 60 ya muda wanaoupata
katika kufanya miradi mikubwa. Fanya maamuzi hata kama muda ulioupata ni
mdogo. Usisubiri muda maalumu. Ukisubiri huo muda hautatokea.
- Weka
kipao mbele kazi zako. Andaa orodha ya
yale mambo unayoyafanya kwenye orodha A na B. Orodha A iwe na kazi ambazo
lazima uzifanye. Na orodha B kazi ambazo unazotaka kuziona zinafanyika. Ni
muhimu kumaliza kazi za orodha A ndio uingie orodha B.
2.
Sina Pesa za kutosha:
Changamoto nyengine inayowasumbua watu wengi ni kusema kwamba hana pesa za
kutosha. Ili kuondokana na changamoto hiyo kwanza achana na hiyo dhana ya
kusema huna pesa za kutosha. Unaposema hivyo unakuwa tayari umeyaingiza mawazo
hasi kwenye kichwa chako. Hata kama ni kweli huna pesa kwa wakati huo. Lakini
ni lazima uwe na fikra tofauti. Kumbuka mawazo yako ndio vitendo vyako. Hivyo
ni lazima ufikirie njia na mipango ya kuwa huru kifedha.
3.
Nahitaji Kuboresha Afya Yangu: Sote
tunajuwa kwamba ili tuwe na afya bora tunahitaji kufanya mazoezi. Tunahitaji
kula vizuri na tunahitaji kulala vizuri.
Ili uweze kutatua changamoto hii
unahitaji kufanya yafuatayo;
- Panga
Ratiba ya Kufanya Mazoezi: Hakikisha unatenga
muda maalumu kwa ajili ya mazoezi. Mazoezi yatukufanya kuuweka mwili,
akili na kiwiliwili kwenye hali mzuri ya kiafya. Na kwa siku dakika 20
zinatosha kufanya mazoezi. Unapofanya mazoezi kila siku utaufanya mwili
wako uwe na afya ilyo bora na maisha yako yatakuwa tofauti sana.
- Boresha
Mlo Wako: Unaweza kuboresha mlo wako kwa kuachana na
vyakula na vinywaji ambavyo havina lishe bora. Punguza matumizi ya kunywa
soda. Kunywa maji ya kutosha. Ongeza matunda na mboga mboga kwenye mlo
wako.
- Lala Zaidi: Wataalamu wanashauri kulala kati ya masaa 7 hadi 8 kwa siku. Vile vile napenda kukushauri kuangalia ubora wa usingizi wako. Nakushauri ulale kabla ya saa 6 usiku. Nakushauri usile usiku sana. Kufanya hivyo itakusaidia ulale usingizi ulio bora.
Afya yako ndio kiungo muhimu cha
mafanikio yako. Hivyo ni lazima ujali afya yako kwa mafanikio yako.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena