Biashara ni
shughuli ambayo unaweza kuifanya na ukaweza kuingiza kipato. Biashara yoyote
ile inahitaji usimamizi mzuri ili iweze kusimama na kuleta mafanikio.
Watu
wengi wanapoamua kuiingia katika biashara wanakosa muda wa usimamizi wa
biashara zao. Badala yake wanaajiri wafanyakazi kwa ajili ya usimamizi huo.
Wapo
wafanyakazi wazuri wenye usimamizi mzuri na wanaoweza kuendesha biashara hiyo
vizuri. Wanaoweza kuendesha biashara kwa ustadi mkubwa bila ya kuwepo
na mmiliki wa biashara. Lakini pia wapo wasimamizi wasiojali umuhimu wa
biashara yako. Watu wasiojali umuhimu wa biashara ni rahisi kuiangusha biashara
na kuipatia biashara hasara kubwa.
Sio vibaya
kumuweka mfanyakazi aendeshe biashara yako. Lakini umakini mkubwa
unahitajika katika usimamizi ili biashara yako isiendeshwe kwa hasara.
Usimuamini mfanyakazi wako kwa asilimia mia moja. Vile vile usimpe mfanyakazi
wa biashara yako usimamizi na kuchukua maamuzi asilimia zote. Kufanya hivyo
utakuwa unaichimbia kaburi biashara yako.
Watu wengi
wamekuwa na wanaendelea kulizwa na wafanyakazi wao. Tumeona wafanyakazi
wengi wakipotea na mtaji na pesa za biashara. Tumeshuhudia wafanyakazi
wengi wanasababisha hasara kila siku katika biashara. Wafanyabiashara kila siku
tumeona wakilalamika kuhusu usimamizi na uendeshwaji wa biashara zao.
Ndugu
msomaji wa Makala hii. Zifuatazo ni mbinu za
kufuata zitakazokuwezesha kuondokana na changamoto ya usimamizi
wa biashara yako.
1.
Usimuamini
mfanyakazi asilimia mia moja: Mfanyakazi unapomuamini na kumfanya yeye ndiye
msimamizi mkuu wa bishara yako ni lazima apoteze mali yako. Hakikisha unatumia
muda angalau saa moja kwa siku kuwepo kwenye biashara yako. Na hii itakusaidia
kujua kinachoendelea kwenye biashara lakini pia itakusidia kujua wateja wako.
2.
Andaa
mpango utakaokusaidia kuhakiki biashara yako: Hakikisha una mpango sahihi.
Mpango utakaoweza kufanya uhakiki na tathmini wa biashara yako. Unaweza
kufanya uhakiki kila wiki mara moja. Mpango huo lazima uwezeshe kujua faida,
mapato na matumizi.
3.
Weka
kumbukumbu: Weka kumbukumbu ya kuandika kila kinachoingia na kila kinachotoka. Hata
kama wewe mmiliki ndio umechukua pesa au bidhaa hakikisha unaiandika. Hakikisha
unaweka kumbukumu ya madeni yote.
Hayo ndiyo mambo ya
msingi katika biashara yako. Ukiyafuata utaweza kuepukana na changamoto za
kupata hasara kwenye biaashara yoyote unayoifanya
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena