Dhamana ni
ile hali au jambo la heshima ambayo mtu huipata au kupewa na mtu au watu
wengine. Dhamana inajenga uaminifu baina ya muhusika na wahusika.
Dhamana
inaweza kuwa ni pesa. Inaweza kuwa cheo, uongozi , amana au jambo lolote lile
linaloleta sifa ya uaminifu. Unapopewa dhamana tayari unakuwa umeaminiwa. Hivyo
ni lazima uwe muaminfu na hapo ndipo kila kitu kitaenda sawa.
Kosa moja
kubwa ambalo watu wanalifanya wanapopewa dhamana ni kukosa sifa ya uaminifu.
Tumewaona
watu wengi wanakabidhiwa pesa kwa ajili ya kufanya miradi mbali mbali.
Wengine wanapewa pesa kwa ajili ya kufikisha sehemu husika. Watu wengine
tumeona wanakabidhiwa pesa kwa ajili ya kuwahudumia watu wengine . Mwisho wa
yote pesa wanakula na kila kitu kinasimama.
Watu wengi
tumewaona wanapokuwa na dhamana ya cheo cha kuwaongoza watu. Ili wafikie
mafanikio ya taasisi wanakosa uzalendo wa kuongoza. Wanakosa
utu, wanakosa uaminifu, wanakosa maadili ya kuongoza. Na mwisho wanakutana
na changamoto ya kufukuzwa kwenye cheo alichonacho.
Kuna
wengine wanapewa mamlaka ya kusimamia maamuzi ya watu. Wengine lakini wanatumia
mamlaka yao vibaya katika kutoa maamuzi sahihi. Watu hawa hawafuati sheria
zilizowekwa. Wao wanatumia mamlaka waliyonayo kwenye kupindisha sheria. Mwisho
wa yote maisha yao yaanaishia pabaya.
Unapokosa
dhamana tayari unakuwa umepoteza sifa ya kuaminiwa. Iwe ni kwa mtu mmoja mmoja
jamii na hata taasisi. Kama ulikuwa ni kiongozi wa siasa. Au dini, kampuni
au taasisi yoyote ile ni vigumu kurudisha sifa uliyokuwa nayo.
Kuwa na
tamaa ya kutaka kupitia njia fupi kujipatia mafanikio. Njia hiyo ndio
msingi wa chanzo ya kosa hili kubwa ambalo watu wanalifanya.
Huwezi kuwa
na maisha mazuri kwa kutegemea mafanikio ya udanganyifu. Huwezi kuwa na maisha
mazuri kwa kudhulumu watu. Na huwezi kuwa na maisha mazuri pasipo na kutenda
haki.
Unapofanya
kosa hili la kukosa dhamana. Ni lazima utapambana na changamoto ya kufukuzwa au
hukumu ya kifungo . Na mwisho wa maisha yako yatakuwa ni mabaya. Unaweza
kukumbwa na matatizo ya msongo wa mawazo. Unaweza kupatwa na pressure na
magonjwa mengi hatarishi kwa maisha yako.
Ili kuweza
kuepuka changamoto hii unatakiwa utumie mamlaka uliyopewa kwa uaminifu.
Kufanya hivyo unaweza kuishi maisha ya amani na yenye furaha daima.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena