Jumanne, 27 Septemba 2016

Unachokitaka ndicho utakachokipata

Kuna msemo usemao kama mlango mmoja unapofungwa basi mwengine utafunguliwa. Chochote unachokiona kama hatari kwako basi kitu hicho ndicho kitakachogeuka na kuwa fursa.

  Unaweza kuona maajabu kwamba ulichokuwa unakitaka kinakusubiri, kinasubiri muda ufike kiweze kutokea. Mapumziko ya kusubiri kutokee ni kwamba huwa kinaruhusu kujipanga kwa moyo, mwili na akili kuungna ili viweze kufanya kazi kwa pamoja. Na maisha ni kama mwalimu anayekuongoza pale ambapo hapajakaa sawa. Kama bado una mawazo ya kizamani ni vugumu sana kusogea.

Na hizi hapa ni baadhi ya dondoo zitakazokufanya mipangilio yako ibadilike na kupata kile unachokitaka.

1. Badili maisha yako Maisha siku zote yanakupa fursa ya kuweza kubadilika. Siku zote zungumza maneno chanya na maneno ya ukweli. Zungumza maneno n'a fanya yale mambo yatakayopelekea hisia chanya kwenye moyo wako.

2. Tambua kama wewe ni wanaadamu Jinsi unavyoweza kujibadili ndivyo hivyo hivyo unavyoweza kuona yale unayoyataka kwa sasa. Jiongezee uwezo wako wa kufikiri, Kubali maumivu utakavyoweza kuyapata. Kubali kufanya kazi kwenye mazingira hatarishi. Jitoe kwenye ile hali ya ukawaida.

3. Tafuta mwuongozo utakaopelekea kutenda. Upo hapa duniani kwa ajili ya ushindi, ushindi utakaokupa fursa za kuweza kuona mafanikio. Kitu chochote ambacho una mtazamo nacho ndicho kitakachokutokea. Hivyo jiweke sawa kwenye vitendo vyako.

4. Penda kudadisi Ili uweze kutambua ukweli kuhusu maisha yako, inahitaji kuvumbua ukweli wa maisha yako. Chochote unachofanya kifanye kama wewe ndivyo. Mabadiliko yanayokutokea kutokana na dhana inayoendana na mtiririko wa maisha, kama tunakuwa Watu wa kulazimisha, kulaumu au tunakuwa Watu wa kujiwekea vikwazo basi hakuna mabadiliko yatakayitokea.

5. Jitambue Juwa wewe ni nani na unataka nini na vitu gani vinakupa msukumo wa kukuongoza. Unaweza kutaka muda wa utulivu kutafuta jibu hili. Unapojitambua utaweza kupata njia ya kuelekea na kufika matarajio yako.

  6.Fumbua macho yako Shukuru kwa Kila jambo linalotokea. Hata kama mawazo yako yatakupeleka kwenye mtazamo mbaya. Jifunze kuiona hali hiyo kwamba haiko sawa. 7. Mimi Kama hujawaza kufika pale unapopataka kwa sasa hiyo isikukatishe tamaa. Vitu huwa vinachukuwa muda ili viweze kutokea. Ni hali ya kawaida kuanguka na baadaye kusimama tena. Mtoto huwezi kuachana na kutembea tena pale anapoanguka, ataendelea mpaka aweze kufanikiwa kutembea. Kuwa binaadamu ni safari tunayotakiwa kuizoeya. Lakini Zawadi ya kweli na ambayo ndiyo moyo ni ule uwezo wa matokeo.
Share:

Jumatatu, 26 Septemba 2016

Jinsi mtazamo wako unavyoathiri maisha yako

Jinsi Mtazamo wako unavyoathiri maisha yako na jambo muhimu la kufanya Mtazamo wako ndio utakaokufanya kuweza kufikia mafanikio unayoyataka.

Sote tunapenda tufanikiwe, tunapenda maisha mazuri, tunapenda kuwa matajiri, tunapenda ushindi, tunapenda familia mzuri hata kazi mzuri.

Tunadhani vyote hivyo vinakuja kwa bahati. Kama tuna mtazamo wa dhana ya kupata bahati basi tutakuwa tunakosea. Ili mambo yetu yawe mazuri kwenye eneo lolote la maisha ni lazima tuangalie mtazamo wetu.

Kama tunapenda kulaumu Kila kitu au Kila mtu kutokana na kufeli kwako, kufanya hivyo hutoweza kufika mafanikio katika maisha. Mtazamo wako unaweza kukufanya usiweze kuona jibu sahihi na mwelekeo sahihi kwa sababu akili yako tayari ina mtazamo hasi na sababu zisizoisha za kufeli. Mtazamo wako ni mawazo ambayo yako kichwani mwako ambayo hubadili akili yako inayopelekea uwezo wa kutenda.

Kama unataka maisha yako, mipango na malengo yako au matokeo yako kuwa chanya, anza kuangalia mtazamo na tabia yako.

Na mtazamo wako ni rahisi kuutathimini. Kitu unachoweza kufanya ni kujiangalia sasa. Au njia nyepesi ya kufanya ni kuangalia watu wako wa karibu wanakuchukuliaje. Watu wako wa karibu ndio kioo chako. Kama wanakupa sapoti basi ujue mtazamo wako uko sahihi na kama wanadharau kwa yale unayoyafanya ujue mtazamo wako hauko sawa.

  Mtazamo unaoujenga ndio unaorudi kwako. Hivyo hakikisha unajenga mtazamo mzuri. Mtazamo wako ni kama usukani kwenye gari. Kama dereva wewe ndiye muhusika wa usukani, na hii ni sawa na mtazamo wako unaweza kuongoza kwenye mwelekeo unaoutaka.

Kumbuka mawazo yote unapoendesha yanakuwa makini kiasi kwamba unahakikisha uko sawa muda wote.. Jiulize kwa nini unafanya unachofanya.

Ni kitu gani kimekuhamasisha ni kwa jinsi gani unafanya unachofanya ? Watu wengi wanashindwa kujibu hili suali. Matokeo yake wanaendelea kufanya kwa mazoeya kufanya kile walichozoeya kufanya na kujiona wapo sahihi. Hapa tunajifunza kwamba watu wengi wana nguvu ya kutaka kufanya, wanajua wanachokitaka lakini hawana nia ya kweli ya kukamilisha kile wanachokitaka.

Sio Kila kitu katika maisha kina urahisi, kuna wakati utapitia kwenye matatizo na changamoto nyingi kwa kile unachokitaka. Mfano watu wengi tunataka tuwe na uhuru wa kifedha lakini ni ukweli usiopingika kwamba mtazamo ndio unafanya vitu vitokee, na hii ndiyo inayotafautisha watu wenye shauku ya kutaka na wale wale wanaoishia njiani kwa kukata tamaa.

Ni lazima ujue ni eneo lipi kwenye maisha linakuwa ndio kikwazo cha wewe usiweze kupata kile unachokitaka. Na kama unataka kufika kwenye hatua mzuri ya kifedha ni lazima uvuke vikwazo vya nyuma. Matatizo yako ya nyuma hakikisha hayana athari yoyote na mafanikio yako unayoyataka sasa. Jaribu kutafuta suluhu ya matatizo yako katika kuyaangalia matatizo katika mtazamo mpya.

Ali Khamis 0784498867
ali76khamis@yahoo.com
Share:

Alhamisi, 22 Septemba 2016

Maisha na Mafanikio

Mafanikio yapo ndani ya uwezo wako.
 Sisi sote tuna uwezo wa kubadili hali iliyopo sasa. Kama unataka kwenda mbele kwenye hali ya kifedha katika maisha yako basi unao uwezo wa kufanya hivyo. Lakini cha kwanza kabisa na cha muhimu unatakiwa kufahamu kwamba uwezo unao na hilo ndilo jambo linaloweza kukuchagulia mwelekeo inaohitaji kuufuata. Sasa kama umeshalijua hilo fikiri ni kitu gani una uwezo nacho.?
Uwezo wako si tu kufika mahala bali pia ni kuanzisha njia, mwenendo na hata vitendo vitakavyousaidia kufika safari yako. Unapoweza kumudu eneo moja kwenye maisha yako hiyo ni ishara ya kuliendea eneo jengine jipya na hii ndio maana hatufikii uwezo wetu. Usiwe unafanya makosa pale unapoweza kufanikiwa baadhi ya malengo yako uliyojiwekea kwamba ndio umeweza kuufikia uwezo wako. Unapofanya hivyo utakuwa inakupa tafsiri isiyo sahihi itakayopelekea kupoteza yale malengo yako makubwa ambayo hujaweza kuyafikia. Watu wengi huwa wanajifunga wao wenyewe katika fikra hii ya mafanikio waliyoyapata nyuma na kufikiri kwamba tayari wamefika.

Jee umejifunga wewe mwenyewe usiwe na upeo wa kufikiria uwezo wako ? Unafikiri ya kwamba tayari umefika uwezo wako? Kama jibu ni ndio basi hiyo ndiyo sababu ya wewe mpaka sasa hujafika kule unapotaka kufika kwenye maisha yako aidha iwe ni kifedha ama kibinafsi.
Uko wapi uwezo wako utakaokufanya ufuate njia ya mafanikio inayoihitaji ? Kumbuka kwamba uwezo wako haujafungwa na wala sio kitu kilichojificha kwamba inahitaji uletewe tochi kukitafuta bali tambua uwezo wako tayari upo nao muda wote. Ni vugumu kuligundua hilo lakini tambua kwamba uwezo wako uko nao muda wote. Unapoamini kwamba una uwezo unapaswa kufanya kutokana na ujunzi ambao una uwezo nao Ili kuweza kufikia kile unachotaka, basi ushauri wangu ni kwamba weka lengo na fanya na hakuna kurudi nyuma.
Mpaka sasa nadhani umeshaelewa kwamba unao uwezo wa kufika mafanikio kwenye maisha. Napenda niseme tena ya kwamba tunatakiwa kuelewa kwamba hatujafika mwisho wa uwezo wetu .Na fikiria ya kwamba kama tutafika pointi ya kwamba hatuwezi kufika tena au hatuwezi kukua tena itakuaje ? Kitu ambacho nakushauri ni muhimu kukifanya kwa sasa ili uweze kukuza uwezo wako ni kwamba usisimame kusoma, ili kuweza kuona uzoefu wako unakuoeleka wapi katika kufikiri mbali zaidi.
Mara nyingi Unapopata uzoefu mpya ndivyo hivyo hivyo utakavyoweza kupata uzoefu ili uweze kuyafika mafanikio. Hii ina maana ya kwamba uwezo hauna mwisho kwa sababu tunavyokua na ndivyo uzoefu unavyokua. Kila siku tambua kwamba una kitu cha kujifunza na ndivyo hivyo hivyo unavyokua. Na hapo ndipo unapoweza kutumia ujuzi ulioupata ili uweze kufanya vizuri zaidi katika siku yako inayofuata na kuendelea.
Kila siku mpya inajengwa kutokana na siku iliyoisha na hii ndiyo inayotufanya tuwe karibu na uwezo wetu wa kila siku. Usifanye makosa kwa kuangalia hali ya sasa na kufikiri kwamba katu hutoifikia shauku yako. Ifanyie kazi siku yako ya leo kwa kiwango cha juu, hii itakusaidia kufanya vyema zaidi kesho. Wakati unapotaka kuwa na mafanikio unatakiwa kufahamu njia za mafanikio, njia ambazo mawazo yako hayakuweza kufikiria kabla ya hapo.
Ali Khamis 0784498867
 ali76khamis@yahoo.com
Share:

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA