Jumatano, 2 Novemba 2016

Fahamu Mambo Makubwa Yanayoweza Kukuvuusha Kwenye Mafanikio

 
Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo makubwa yanayoweza kukuvuusha kwenye mafanikio.

Ni mara nyingi tumeona watu wakitengeneza lawama kwa kila mtu anapofanya makosa. Ili tuweze kutimiza malengo yetu,  hatuhitaji kuishi kwa kutegemea kwamba wewe uweze kuwashinda watu wote. Kwenye maisha kila mtu ana mapungufu yake, hivyo usichukulie uzaifu wao kama silaha yako ya kuwahukumu wengine. Kama tutaangalia mtazamo wa maisha ni vyema kuangalia udhaifu wako kuwa ndio kigezo sahihi cha kuimarisha mafanikio yako.

Haya hapa ndio mambo ambayo ukiyafanya yatakupeka kwenye mafanikio unayoyataka.

1.           Tengeneza Mfumo Wako Wa Maisha
Tengeneza mfumo ulio imara ambao utakuwezesha kuishi maisha yako. Jifunze uwezo wa kuwa jasiri wa kufuata mapenzi na hisia zako zinavyokuongoza. Tengeneza hadithi ya maisha yako. Na kuweza yote hayo ni lazima ukubali kwamba uzaifu wako ndio nguvu yako ya kuimarisha mafanikio yako.

2.           Kufeli Ni Mwalimu Mzuri
Watu walioshinda kwenye maisha yao walifanya kazi ngumu ya kutafuta mafanikio, lakini pia walipuuzia kushindwa. Waliweza kuwa wajasiri na hawakukata tamaa. Ni muhimu kuelewa kwamba kufeli ni mwalimu mzuri. Huwezi kufanikiwa bila ya kupitia njia ya kufeli. Na huwezi kufanikiwa kama hujajifunza kotokana na kufeli. Kuwa na muda wa kutosha wa kuweza kujifunza kutokana na makosa unayofanya.

3.           Jiwekee malengo Makubwa
Malengo na mipango yako unayopanga katika maisha ni muhimu yawe makubwa. Kama unataka kupata mara kumi basi ni vyema kupanga kupata mara mia moja. Ukipanga kupata mambo makubwa kutakusaidia kutimiza ndoto zako. Unaweza kufanya kazi kwa bidii na kufanya kila njia ili kuweza kufikia malengo yako. Unapopanga kufanya mambo makubwa hutoweza kuogopa kushindwa.  Ukiweza kuweka ndoto kubwa utafanya kila linalowezekena kufanikisha na kutafuta uzoefu wa kutosha.

Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo. 

 

 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA