Habari za leo ndugu msomaji wa
nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu
za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha. Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na makosa unayotakiwa
kuyaepuka ili uweze kufikia malengo na ndoto zako katika maisha.
Haijalishi umejiwekea malengo
yenye ukubwa gani au udogo kiasi gani, lakini ukweli ni kwamba unahitaji
dhamira, lengo, kufanya kazi kwa bidii, ujasiri na uamuzi wa kufanikiwa. Hakuna
njia ya mkato yenye matumaini ya kuleta mafanikio kwenye malengo yako bila ya
kupitia mambo haya muhimu. Watu wengi linapokuja suala la malengo huwa
tunafanya na tunapofika njiani tuacha kufanya kwa sababu ya ugumu wa kufanya.
Unapoamua kuianza safari yako ya
mafanikio epuka kufanya makosa haya matano ili uweze kuongeza nafasi yako ya
kufikia ndoto na lengo ulilojiwekea katika maisha.
1.
Epuka Kutarajia Matokeo Ya
Haraka
Kosa hili linaweza kuwa na
athari kubwa kwenye Imani yako na matarajio ya kufanikiwa. Kama unaweza
kutarajia matokeo ya haraka kinachotokea ni kupoteza dira na muelekeo wa
kufikia ndoto na lengo lako ulilojiwekea. Linapokuja jambo la malengo unahitaji
kuwa na uvumilivu wa hali ya juu. Uvumilivu wako ndio utakaokufanya kutimiza
safari yako ya mafanikio.
2.
Epuka Kuwa Na Mtazamo Wa
Kushindwa
Ni kosa kubwa kukubali kwamba
umeshindwa zaidi ya mara moja na kwamba sasa huwezi kusimama tena na kuanza
upya.
Ili uweze kujimudu kwenye maisha
yako ni pale unapokabilana na kushindwa. Ni wewe ndiye utakayeamua ni jinsi
gani kushindwa kunaweza kuathiri maisha yako. Unaweza kuamua kushinda au uamue
kukata tamaa.
3.
Epuka Kushindwa Kwa Kutarajia Au
Kupangilia Yasiyotarajiwa
Kwenye malengo yetu tutarajie
kupata ambayo hatujatarajia kuyapata. Ni kawaida kwetu tunapokutana na mambo
ambayo hatujayatarajia tunaona kwamba kila kitu kimeshakuwa hakiwezekani. Njia
mzuri ya kufanya tunapopanga malengo yetu ni kufanya maandalizi kwa ajili ya
mambo tusiyoyatarajia.
4.
Epuka Kuchoka Njiani
Kwa ajili ya kupata kile
unachokitaka kwenye maisha yako ni lazima ubadilike, fanya vitu kwa utofauti,
tengeneza tabia mpya na mawazo mapya. Na vyote hivyo haviwezi kuja kwa usiku
mmoja. Vitu hivyo vinatokea kwa kuendelea kuvirudia kila siku. Jiandae na hali
itakayojitokeza ya kutokujisikia kufanya. Inapojitokeza hali hiyo ni muhimu kuendelea
kila siku mpaka utimize ndoto uliyojiwekea.
5.
Epuka Kujilinganisha Na Wengine
Kitendo cha kujilinganisha
maisha yako na wengine kitakufanya usiweze kufanya vyema katika malengo yako.
Usichukulie kufeli kwa mtu mwengine kwamba na wewe ndio huwezi kufikia ndoto
zako na malengo yako. Tambua kwamba watu hatulingani na inawezekana nyote
mukawa na lengo na ndoto za aina moja lakini mafanikio yakawa tofauti kabisa.
Unapoweza kuepuka makosa haya
matano utaweza kutimiza malengo yako, utakuwa na nidhamu mzuri, utaweza kuwa
jasiri na utakuwa na msimamo utakaoweza kukusaidia kufanikiwa katika mambo yote
ambayo unataka kufika katika maisha yako.
Weka email yako hapa na bonyeza
SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena