Jumamosi, 17 Desemba 2016

Fahamu Umuhimu Wa Kujiwekea Malengo Makubwa Kwenye Maisha Yako



Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na umuhimu wa Kujiwekea Malengo Makubwa.

Watu wengi katika dunia ya sasa tunaishi bila ya kuweka malengo. Watu wengi tunaishi kwa sababu tu tupo tumezaliwa tunatakiwa kuishi. Tukifanya tathmini ya watu ambao wanajiwekea malengo kwenye maisha yao ni ukweli usiopingika kwa hawatazidi asilimia kumi. Sababu kubwa ya watu kutoweka malengo ni kuwa hawana uhakika wa kile wanachokifanya. Hajui anafanya nini sasa, atafanya nini kesho na anataka kufanya nini kwa muda wa mwaka mzima.

Ndugu yangu kuweka malengo inakupa muda wa kujitathimini kwenye maisha yako kwa ujumla. Kuweka malengo inakusaidia kujua kama unaenda mbele kwenye maisha yako ama unarudi nyuma. 

Kwa nini unahitaji kuweka malengo makubwa kwenye  maisha yako?

Zipo sababu nyingi ni kwa nini unahitaji kuweka malengo makubwa lakini kwa leo nitakupa sababu hizi tano(05): 

1.           Fahamu kwamba uwezo unao mkubwa.  Uwezo unao mkubwa lakini mpaka sasa hujaweza kuutumia. Kama uwezo wako ulionao unaendelea kuutumia katika kufanikisha malengo ya watu wengine ni bora kuanzia leo ukafikiria njia tofauti na hiyo. Maana nikuambie rafiki yangu kama unaishi kwa kufanikisha malengo ya watu wengine basi akili yako unaidumaza. Eti unajipa sababu ya kwamba mimi nimesoma ili niajiriwe. Tabia hiyo inakujenga usiweze kufikiria njia nyengine inayofaa na uwezo wako mkubwa ulionao. Jiandae kutoka huko ili uweze kuutumia uwezo wako mkubwa ulionao.

2.           Fahamu Kwamba Unastahili Kuishi Maisha Bora. Hukuzaliwa kufanya kazi ambayo huipendi, hukuzaliwa kutumia muda wako wote kwenye utumwa. Umezaliwa kuwa na maisha bora na ya kipekee. Tumia uwezo wako na kipaji chako na fanya kitu ambacho unakipenda kwa ajili ya kuishi maisha bora. Huwezi kuwa na maisha bora kama utashindwa kufanya kitu ambacho unakipenda.

3.           Fahamu Muda Na Pesa Ndio Rasilimali Muhimu Kwako. Wezi ni wengi, usumbufu ni mwingi na kila mtu anawinda rasilimili zako.  Usikubali kila mtu awinde hela zako na muda wako. Hizo ndio rasililimali zako ambazo zinakuwezesha kupanga mambo makubwa yanayotoa uzalishaji bora na maisha yatakayokuletea mapinduzi makubwa.

4.           Weka Malengo Yasiyo Ya Kawaida. Fahamu wewe ni wa pekee, Huna sifa ya kufanya kile ambacho kila mtu anakifanya.  Unatakiwa uwe tofauti na mkumbo wa watu. Weka dhamira ya kweli ambayo yataweza kukutofautisha wewe na wengine na kukufanya kuwa mbali na kawaida. Usifanya kwa sababu eti jana nimefanya bali fanya kwa sababu umeamua kufanya kutokana na malengo uliyojiwekea ambayo siyo ya kawaida.

5.           Fahamu Kwamba Unahitaji Kwenda Mbele Na Sio Kurudi Nyuma. Jipe uhakika kwamba hakuna kitu ambacho kinaweza kukuzuia kusimama kuanzia sasa. Anza hapo ulipo sasa na usisisubiri mpaka ukamilishe mtaji. Muda sio rafiki sana na saa zinaenda kwa kasi ya ajabu.  

Hayo ndio mambo matano ambayo nimekuandalia kwa leo msomaji wangu na mfuatiliaji wangu mzuri wa Makala zangu. Nakuahidi sitokuangusha nitakuletea kile kilicho bora kwa mafanikio ya maisha yako. Hivyo endelea kunifuatilia na kusoma Makala zangu zenye kuleta hamasa na ubora wenye mafanikio. Sitokubali kamwe kukuacha hivi hivi. Tutakuwa wote hadi kilele cha mafanikio. 


Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako. 

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
0784498867 

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA