Habari za leo ndugu
msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa
makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.
Leo hii napenda
kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na upandaji wa mbegu bora kwa
ajili ya maisha yako ya mafanikio.
Kuna Msemo wa Kiswahili
unasema upandacho ndicho uvunacho. Msemo huu una maana mzuri na ni muhimu
kuufahamu. Mkulima siku zote anapopanda mahindi anategemea avune mahindi,
Huwezi kupanda mahindi na ukavuna nyanya.
Mbegu bora ambayo
utaipanda leo kwenye maisha yako ni msingi mzuri kwa maisha yako ya baadaye.
Sasa ni uamuzi wako wa kuamua kupanda leo kile ambacho utavuna kesho.
Kitu ambacho kipo karibu yako ni kupanda kwenye udongo bora wenye rutuba.
Baada ya hapo hakikisha mbegu yako inapata virutubisho vya kutosha. Mbegu yako
inahitaji upendo, mbegu uliyoipanda inahitaji muda, inahitaji kuvumilia na
inahitaji uwezweshaji wa kutosha ili iweze kufanya vizuri.
Kumbuka kwamba mbegu
ndogo inaweza kuleta mazao mengi. Kama ni mtoto basi anaweza kuwa bingwa
kwenye hii dunia. Mbegu mia za papai unaweza kutoa mapapai zaidi ya elfu moja.
Unapoweza kuongeza ukubwa wa unachofanya ndivyo hivyo hivyo unavyoweza kuongeza
mafanikio ya maisha yako.
Hakuna ambaye anayeweza
kutengeneza mafanikio yako , na hakuna mtu ambaye anaweza kuongoza maisha yako
pasipo kuwa na ridhaa yako ya kutaka. Na hakuna ambaye anao uwezo wa
kukusimamisha wewe usifanikiwe. Juhudi zako na maarifa ziweke kwenye
eneo ambalo litakuletea mafanikio. Usifanye kitu ambacho hakitaweza kuleta
mafanikio yako. Jiandae kupanda mbegu ya mafanikio mara elfu moja zaidi.
Siri ya mafanikio yako
imefichwa na kile unachokifanya kila siku. Jinsi unavyoweza kutatua
matatizo ya wengine ndivyo unavyokaribisha mafanikio yako.
Weka email yako hapa na
bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email
yako.
Karibu Kwenye Blog Yako
Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
0784498867
0 comments:
Chapisha Maoni
Asante Sana Na Karibu Tena