Ijumaa, 2 Desemba 2016

Mambo Sita (06) Muhimu Ya Kufanya Kwa Ajili Ya Kukuletea Hamasa Ya Mafanikio



Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo muhimu ya kufanya kwa ajili ya kukuletea hamasa ya mafanikio.

Hamasa ni chachu ya mafanikio. Katika maisha ni muhimu kufahamu njia zitakazoweza kukupatia shauku ya mafanikio, njia zinazoweza kukupa msisimko. Hakiksha unayajua mambo muhimu yanayoweza kukukumbusha kila siku katika kukuwezesha kuwa na hamasa ya mafanikio ya maisha yako.

1.           Fanya Kitu Ambacho Sio Cha Kawaida Kwako.
Kwenye maisha ni lazima uamue kufanya maamuzi ambayo yataweza kukufikisha kileleni. Nafikiri mpaka sasa unapoendelea kunasoma Makala hii umeshafikiria ni jambo lipi kubwa unaweza kulifanya kwenye maisha yako. Jambo hilo nina uhakika lipo kwenye akili yako. Kama tayari hakikisha unalifanya kwa umakini wa hali ya juu na kuweka juhudi zako zote.

Kumbuka maisha ni kama kivuli ambacho kiko kwenye kiza. Mara unapoamua kwamba sasa nataka mabadiliko na kwenda kwenye mwanga, na hapo ndipo maisha yako yatakapoanza kuwa tofauti na ya kushangaza. Hivyo kila unalolifanya lifanye kwa kiwango cha umakini wa hali ya juu.

2.           Tambua Vikwazo Vyako.
Ni muhimu kujua vitu ambavyo ni vikwazo kwako. Tambua mambo ambayo yanaweza kukurudisha nyuma. Gundua mambo ambayo yatakupelekea wewe ukwame. Ukiweza kujua vitu ambavyo vitakupelekea wewe ukwame itakurahisishia kuona njia ya kutatua mambo yanayoweza kukukwamisha.

3.           Kuwa Na Watu Sahihi.
Hakikisha watu wako wa karibu wanakuwa na mtazamo chanya dhidi yako. Ni muhimu watu wako wawe na malengo mazuri kwenye maisha yao. Zingatia kuchagua marafiki ambao wana mtazamo wa mbali kwenye maisha wanayoishi. Epuka kuwa na marafiki wenye mtazamo hasi. Achana na watu sumu wenye kulaumu kwa kila jambo.

4.           Yajali Maisha Yako.
Chukua tahadhari kubwa kuhusiana na afya yako. Kula vizuri na fanya mazoezi. Hakikisha unakula chakula kizuri kwa ajili ya kuimarisha afya yako. Fanya kazi endelevu na kuwa na muda wa mapumziko. Hakiksha unalala mapema na kuamka mapema.

5.           Jione Wewe Kuwa Ndiye Bora.
Katika eneo lolote ulilochagua kwenye maisha yako hakikisha unafanya kwa kiwango cha juu. Na jambo lolote unalolifanya elewa kwamba linaanzia na mawazo yako.

6.           Endelea Kusonga Mbele.
Hakikisha chochote unachofanya kwenye maisha yako kinaendelea. Fanya kwa mwendo wa haraka kuhakikisha kwamba unafanya na wala hakuna kitu kitakachokufanya wewe usimame. Jinsi unavyoweza kufanya kwa haraka zaidi ndivyo hivyo unavyojenga misingi ya mafanikio. Kama umepanga kufanya jambo kwa mwaka mmoja hakikisha unalikamilisha ndani ya kipindi cha miezi sita.

Hivyo kama unataka mafanikio ya maisha yako hakikisha unafuta mambo haya sita yatakayoweza kujenga hamasa kwenye mafanikio yako.


Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja  kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
  0784498867
 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

0 comments:

Chapisha Maoni

Asante Sana Na Karibu Tena

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA