Jumanne, 29 Novemba 2016

Fahamu Mambo Magumu Matano (05) Kwa Kila Mfanyabiashara Mwenye Mafanikio Lazima Ayapitie

 
Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo magumu kwa kila mfanyabiashara mwenye mafanikio lazima ayapitie.

Watu wengi wanapaanza kuingia kwenye biashara wanajiona tayari wameyapatia maisha. Wanakuwa na ndoto kwamba ipo siku wataacha kazi wanazozifanya, na kufanya mambo wanayoyapenda na baadaye kuishi maisha ya kifahari.

Kuanzisha biashara ni mchakato mpana wa kuendelea kujifunza unaopelekea kubadili maisha yako. Ni mchakato ambao unaweza kukuongoza kwenye njia ambayo hukuweza kuitarajia na kuweza kufungua milango mipya ya mafanikio yako.

Kuanzisha biashara hadi isimame inahitaji juhudi sana. Inachukua muda wa kujitolea, nguvu na uwezo utakaokupeleka kwenye mafanikio. Ni lazima utakumbana na vikwazo na vikwazo hivyo haviangalii wewe ni nani.

Hivyo tambua kwamba unapokumbana moja ya mambo haya magumu jua kwamba hiyo ni kawaida kwa mfanyabiashara.

1.           Kuna Wakati Utahisi Kuchoka
Watu wanaposema kwamba kujifunza ujuzi wowote kunahitaji muda, wengi wetu tunataka mambo ya haraka. Matokeo yake watu wanapoteza muelekeo njiani na kuamua kufanya kitu chengine .

Kuanza na kubaki kwenye biashara ni sawa sawa na kumudu ujuzi mwengine . Biashara inahitaji uvumilivu na jukumu la kulea na kuikuza. Kuna wakati tunachoka na tunachofanya lakini kuna wakati tunaona mambo yanakuwa mazuri na tunayafurahia. Na hapa jambo zuri unalotakiwa kulifanya ni kubaki na kuendelea unachofanya bila ya kuchoka na kuacha kufanya.

2.           Biashara Inavyoendelea Kukuwa Ndivyo Utakavyokutana Na Changamoto Zaidi
Utapoanza biashara unakuwa na matumaini kwamba kila kitu kitaenda vizuri. Unakuwa na Imani kwamba hakuna kikwazo chochote kinachoweza kukutokea. Lakini hii ni njia ya kujipa matumaini mwanzoni unapoanza biashara. Ukweli ni kwamba biashara yoyote ile ina ugumu wake. Mara unapoanza hatua ya kujifunza jinsi biashara inavyokuwa hatua inayofuata lazima utakumbana na changamoto. Lazima usimame kwa miguu yako na jiandae kukabiliana na changamoto zinazokutokea. Fikiria hatua zitakazoifanya biashara yako kukuwa na fanya mabadiliko kutokana na mazingira yaliyopo.

3.           Wewe Huna Ujuzi Kama Unavyofikiria
Wengi wanapoanza biashara wanashindwa kujua uwezo wao. Wengi wanakuwa na mtazamo kwamba unajua kila kitu. Lakini ukweli ni kwamba huna maarifa ya kutosha kama unavyodhania.

Hiyo ni kawaida ni sehemu ya maisha . Jinsi unavyoweza kuwa na uzoefu kwenye hali zote mbili kufeli au kufanikiwa ndivyo unavyojenga ukomavu. Vile vile ni muhimu kujifunza kutoka kwa wale ambao wako mbele yako.

4.           Lazima Ujipe Kazi Tofauti Tofauti
Kazi nyingi zinahitaji kufanya kitu kinachofanana mara nyingi zaidi. Unapoanzisha biashara kwa upande mwengine maana yake ni kwamba unatakiwa kuelewa kila kitu. Ni lazima umudu maeneo yote ya biashara unayoifanya, na hii itakufundisha mambo mengi. Kuna wakati utajifunza kwenye kujaribu kitu kipya kuna wakati utajifunza kutokana na makosa unayofanya.

Nje ya biashara yako unaweza pia kujifunza kutokana na kusoma Makala na vitabu mbali mbali. Pia utajifunza katika kuhudhuria mafunzo au kuongea na watu wengine. Lakini kusoma ndio eneo ambalo unapaswa ulipe umuhimu wa pekee ili uweze kupata mafanikio unayoyataka kwenye biashara.

5.           Kuna Wakati Unaweza Kukata Tamaa
Nadhani umeshawahi kusikia watu wenye mafanikio wanaongelea kuhusu mambo magumu waliyopitia wakati wanaanza mpaka kufanikiwa kwao. Na wewe tambua kwamba utapitia njia hiyo hiyo. Kuna wakati unaweza kushangazwa kwa nini iko hivyo. Kuna watu watakukatisha tamaa kwa kile unachokifanya. Ikitokea hali hiyo wewe zidisha kufanya.

Tambua kwamba wafanyabiashara wote wametia kwenye hali ngumu kwa njia moja hadi nyengine mpaka kufika hapo walipo. Na kama wewe ni mmoja wao unataka kuwa mfanyabiashara mwenye mafanikio ni lazima uungane nao kwenye mambo hayo magumu waliyoyapitia.

Jiunge Kupata Makala hizi
Weka email yako hapa na bonyeza SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
hudhaifiali@gmail.com
  0784498867

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

Jumapili, 27 Novemba 2016

Ijue Siri Ya Kuwa Mjasiriamali Mwenye Mafanikio


Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na Siri ya kuwa mjasiriamali  mwenye mafanikio.

Jee wewe una ndoto ya kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio? Kama bado una ndoto au tayari umeanza biashara ni muhimu kufahamu jinsi ya kujenga biashara yenye mafanikio na kuelewa zaidi mbinu bora za kiufundi kwenye biashara.

Madhumuni ya kweli na sababu ya kutaka kuelekea kwenye safari yako ya mafanikio ni kufichua kipaji chako kilichojificha. Kila mmoja wetu anacho kipaji ambacho ni muhimu kwa mafanikio yake kama mjasiriamali. Katika safari ya ujasiriamali ni jambo la muhimu kufichua na kukuza kipaji chako kilichojificha.

Kwa kweli kuwa na uwezo wa kufanya mabadiliko na kuleta  athari juu ya dunia lazima kwenda kupitia mfululizo wa majaribio. Majaribio yako yanajiandaa kujenga msingi imara ambao utakuwezesha kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio .

Kuweza kuwa mjasiriamali wa kweli na mwenye mafanikio makubwa lazima ukubali kipaji chako na kiweze kupata ridhaa ya familia na utamaduni wa jamii. Mara baada ya kipaji chako kutambulika katika ngazi ya familia ndio utaanza kuchanua na kufanya makubwa juu ya dunia hii.

Usiwe na hofu katika kuonesha kipaji chako ambacho kinaweza kukusaidia kutengeneza mafanikio ya kuwa mjasiriamali mwenye shauku kubwa ya kufanikiwa. Kimsingi, lengo lako liwe katika kufichua na kukuza kipaji chako ili uweze kuwa na nguvu ya kuweza kutimiza malengo yako.

Unapoweza kuonesha ujuzi wako wa kiufundi na ukiweza kudhibiti hofu yako na kuweza kuondoa vikwazo vinavyokukabili basi mafanikio ya kuweza kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio hakuwezi kuepukika.
Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
0784498867

 

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

Ijumaa, 25 Novemba 2016

Usiogope Kukosea Badala Yake Jifunze Kutokana Na Makosa Unayofanya


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana mafunzo unayoweza kuyapata kutokana na makosa unayoyafanya.

Ni kawaida kwa wanaadamu kufanya makosa kila siku, kuna makosa madogo na makosa makubwa ambayo tunayafanya. Makosa tunayoyafanya ni kama zawadi ambayo hutupatia muongozo wa kujifunza na kutufanya tukuwe kama watu.

Haya hapa ni mafunzo unayoweza kuyapata kutokana na makosa unayoyafanya.

1.           Makosa Yanatufunza Sisi na Yanaweza Kutupa Muongozo Jinsi Tunavyotaka Tuishi. Makosa yanatusaidia kuweza kujitoa. Makosa hutuongoza vile tunavyotaka tuishi. Makosa huweza kutuamsha na kutufanya tuwe makini kwenye mambo tunayoyafanya.

2.           Makosa Yanatufunza Tujikubali. Inawezekena kufurahia makosa yetu na baadaye kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kuyafanyia masahihisho. Yaone makosa kama kituo cha kupumzikia kinachoweza kukupatia nguvu upya baada ya kuchoka.

3.           Makosa Yanatufundisha Namna Ya Kuondokana Na Woga. Kuna wakati unaweza kufanya juhudi zote lakini mambo yanakuwa magumu. Unapoweza kukabiliana na makosa mara nyingi hofu inaondoka.

4.           Makosa Yanatufundisha Jinsi Ya Kuongea Ukweli. Makosa yanatufundisha sisi tuweze kuongea ukweli. Unapofanya makosa na kuweza kukubali mbele za watu makosa uliyofanya inakujenga wewe katika kujifunza zaidi na kupelekea kukuwa.

5.           Makosa Yanatupatia Majibu Ya Kuweza Kujuwa Mambo Yanayoweza Kufanya Kazi Na Yale Ambayo Hayafanyi Kazi. Makosa ni kipimo cha kuweza kufanya uchunguzi. Unapoweza kupata uzoefu wa makosa yanayokutokea unapata ujumbe mzuri wa kugundua kipi kinweza kufanya kazi na kipi hakifanyi kazi.

6.           Makosa Yanatufundisha Kufanya Uadilifu. Mara nyingi makosa yanatutokea pale ambapo tumeshindwa kufuata utaratibu. Na makosa makubwa mara nyingi huanza na makosa madogo. Hivyo ni muhimu kuchunga uadilifu kwa mambo yetu tunayoyafanya siku zote. Makosa ni kama ishara ya maneno na vitendo vyetu kwamba haviendani sawa.

Weka email yako hapa na bonyeza SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
hudhaifiali@gmail.com
       0784498867
 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

Jumatano, 23 Novemba 2016

Zijue Kanuni Tano (05) Muhimu Kwa Ajili Ya Kupata Mafanikio Makubwa Kwenye Maisha Yako


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na kanuni muhimu kwa ajili ya kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako. 

Kila mtu anapenda afanikiwe. Mafanikio makubwa hayawezi kuja hivi hivi tu. Kama unataka kupata mafanikio makubwa, ni lazima ufanje zaidi ya kawaida yako. Ni lazima uchukue hatua kubwa zaidi. Lazima ndoto zako ziwe kubwa zaidi kuliko vile unavyotarajia.

Katika Makala hii nitakuelezea kanuni hizi tano ambazo zitakuweka kwenye njia sahihi itakayokupeleka kufikia mafanikio yako makubwa.

1.           Panga Malengo Yako Kwa Kiwango Cha Juu Unachoweza Kukifikia
Kwanza ni muhimu kuamini kwamba huwezi kufikia mafanikio makubwa pasipo na kuwa malengo uliyoyaweka wazi. Malengo yako ni ule uwezo wako wa kuona sasa hivi pale ambapo unataka kuwa katika maisha ya baadaye. Na hii ndio sababu muhimu ya wewe kuwa ni lazima uwe na ndoto kubwa. Panga malengo ambayo yatakusukuma wewe na kukutoa nje ya ukanda wa faraja yako ya kila siku. Lakini pia ni muhimu kuweka malengo ambayo unaweza kuyafikia ile usiweze kuchoka njiani na kupata msongo wa mawazo. Kama utakuwa umeelewa vizuri basi utakuwa tayari uko kwenye njia ya mafaniko.

2.           Chukua Hatua Ya Kufanya Mambo Makubwa
Kama huwezi kuruka basi kimbia. Kama huwezi kukimbia basi tembea. Kama huwezi kutembea basi tambaa. Lakini njia yoyote utakayopitia iwe ni kusonga mbele. Tambua kwamba haitoshi kupanga malengo pekee bali pia lazima uchukue maamuzi ya kufanya ili uweze kufanikiwa. Unapoweka malengo yako ni muhimu kuweka mfumo wa kukusaidia kuhakikisha kwamba malengo yako yote umeyapanga katika hatua na tarehe ya mwisho ya kuweza kuyafikia. Na kufanya hivyo hakikisha umeyavunja malengo yako katika hatua ndogo ndogo ambazo unaweza kufanya kila siku. Ukiweza kufanikisha mpango wa kwanza nenda kwenye mpango unaofuata. Jinsi unavyoweza kufanikisha malengo yako ndivyo zaidi unavyopata msukumo wa kufanya zaidi.

3.           Kubali, Ongea na Chukua Hatua Kwa Vitendo Kwa Yale Unayoyaamini
Ukitaka kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako ni lazima ufunge mlango wa mawazo yako dhidi ya mambo yote yanayoweza kukukatisha tamaa. Kama utakuwa umefanya uchunguzi kwenye maisha yako ni kwamba utagundua siku zote kama unataka kufikia ndoto kubwa utaona kama akili yako inakwambia kwamba haiwezekani. Lakini ukweli ni kwamba kama unataka mafanikio makubwa ni lazima uende maili ya ziada isiyo ya kawaida. Lazima uiambie akili yako kwamba inawezekana. Zaidi unavyojenga Imani ndivyo hivyo unavyoweza kuondokana na hofu ya kushindwa. Wewe ndiye wa pekee unayeweza kujihamasisha kufikia mafanikio yako na tambua kwamba hawezi kutokea mwengine.

4.           Tenda Kwa Ujasiri Na Uadilifu
Uadilifu ni muhimu sana kama wewe ni mfanyakazi au mwajiri, mwanfunzi au mfanyabiashara. Uadilfu lazima uwe mzima usiogawanyika, uwe na uwezo wa kuzalisha matokeo sawa bila ya kujali mazingira gani uliyopo. Lazima ukuze maadili ya uaminifu na maadili yaliyo imara. Siku zote ukiwa muadilifu basi ujasiri hufuata.

5.           Fanya Ukaguzi Wa Kila Kitendo
Kila hatua lazima iwe na matokeo. Hivyo pima kitendo chako cha kabla na baada ya wewe kufanya ili kujua hasa athari ya tendo juu ya maisha yako na mafanikio. Jambo muhimu la kukumbuka katika vitendo vyako ni kwamba kila kitu kina umuhimu na kila kitendo lazima kilete matokeo.

Unapoweza kupanga mlengo yako kwa kiwango cha juu, unapochukua hatua ya kufanya mambo makubwa, Unapoweza kutenda kwa ujasiri na uaminifu na ukiweza kufanya ukaguzi wa kila tendo unalotaka kulifanya basi utakuwa umeweza kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako.

Weka email yako hapa na bonyeza Subscribe ili kuweza kupokea makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
0784498867 

Jiunge Kupata Makala Hizi

* indicates required


Share:

Jumanne, 22 Novemba 2016

Chochote Unachotaka Kufanya Kwenye Maisha Yako Kinawezekana


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na kufanya chochote unachotaka kufanya kwenye maisha yako kinawezekana.

Unaweza kufanya chochote kwenye maisha yako. Na ukiamua kufanya hakuna unachoweza kushindwa. Tambua kwamba hakuna muda wa kusubiri ili uweze kuanza. Msingi wa yote hayo ni kujipangia malengo na mipango ili uweze kufanikiwa. Na mbinu sahihi ya kufanya chochote unachotaka kukifanya ili uweze kujiletea mafanikio ni kupenda kile unachotaka kukifanya na kifanye kwa furaha. Pia usiruhusu kitu chengine kiondoe furaha yako.

Hizi hapa ni njia sita (06) zitakazoweza kukufikisha kwenye safari yako ya mafanikio:

1.           Jifunze Kitu Kipya
Jinsi unavyoweza kujifunza zaidi ndivyo ambavyo unavyoweza kuongeza maarifa. Unaweza kuona vitu unavyovipenda ni vile vinavyokupatia furaha. Na vitu hivyo ndivyo vinavyoweza kukupatia furaha kwenye maisha yako.

Upo uzoefu ambao hauna mwisho. Fanya mambo mengi tofauti na usipende kujiwekea mipaka.

2.           Andika Ndoto Zako Zote
Andika kila kitu ambacho kipo kwenye ndoto zako na kile unachotaka kukifanya kwenye maisha yako. Hakikisha unachoamua kufanya kinakuletea furaha. Ukimaliza kuandaa orodha yako pangilia upya kile ambacho ni muhimu zaidi na kitu hicho kiwe cha mwanzo kukifanya.

Usiogope kuwa na ndoto ambazo zitakuchukua muda mwingi kuweza kuzikamilisha. Muda ni jambo dogo sana kama utaamua kufanya kitu ambacho unakipenda.

3.           Tengeneza Dira ya Maisha yako
Dira yako itajengwa kutokana na mawazo yako uliyonayo. Na hii ndiyo inayobeba sura mzima ya maisha yako, ndoto zako na mwelekeo wa kile unachotaka kufanya kwenye maisha yako.

4.           Tambua ni Kitu Gani Kinahitajika Ili Uweze Kufika
Ili uweze kufanya kitu chochote unachotaka ni muhimu kujuwa vitu vinavyohitajika kwa ajili ya kuweza kukufikisha huko. Kama ni mafunzo yanahitajika basi hakikisha unapata mafunzo ya kutosha. Kama ni pesa zinahitajika basi usiogope kutumia pesa ili ziweze kukupatia thamani unayoitafuta.

5.           Tengeneza Mpango Kazi Wa Miaka Mitano
Usifikirie kitu pekee cha kukufikisha pale unapotaka kwenda , lakini pia fikiria kuandaa mpango kazi wa miaka mitano  na jinsi unavyoweza kufika. Tengeneza mchanganuo ambao utakuwa na vitu vyote vya msingi. Na hiyo itakuwa ndiyo njia yako itakayokuongoza.

6.           Fanya Hatua Kwa Hatua
Kama malengo yako unayotaka kuyafanya ni makubwa ambayo yatachukuwa muda mrefu, yagawanye sehemu ndogo ndodo ili yaweze kuwa rahisi kuyatekeleza. Na njia hii itakusaidia kukutia hamasa ya kufanya zaidi na kupelekea kufikia mipango yako.

Hakikisha unajua nini unachotaka kufanya na ni muhimu kuandaa mpango kazi ambao utakufikisha na kupata chochote unachotaka kufanya. Usikate tamaa kwenye dunia hii ukiamua kufanya hakuna kinachoweza kukushinda.

Weka email yako hapa na bonyeza SUBSCRIBE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
au
  0784498867 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

Jumapili, 20 Novemba 2016

Fahamu Njia Tano (05) Unazotakiwa Kuziishi Ili Watu Waweze Kukumbuka


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na njia tano unazotakiwa kiziishi ili uweze kukumbukwa kwenye maisha yako.

Kuanzia sasa ni lazima tutambue kwamba tunazo nguvu za kuacha athari chanya kwenye maisha tunayoyaishi katika dunia. Ni lazima kujitoa katika kila nafasi unayoweza kuipata. Ni muhimu kuyafanya maishi yako yawe zawadi. Siku ukitoweka duniani watu wanatakiwa waendelee kukukumbuka wewe kwa yale mazuri uliyoyafanya duniani.

Yapo makundi matano ambayo unaweza kuyafanya ili watu waendelee kukukumbuka kwa mazuri uliyofanya:

1.           Kijamii:  Yaguse Maisha Ya Wengine
Japokuwa kila mtu anakuwa na ndoto zake na matumaini katika maisha. Lakini watu wengi wanakuwa wapo tayari kusubiri na kupokea mabadiliko na ushauri wa maisha kutoka kwa wengine. Kuwa sehemu ya mchango mkubwa kwenye jamii kwa kutoa huduma ambayo itaweza kuwafikia watu wengi zaidi.

2.           Binafsi: Jiangalie Wewe Mwenyewe
Wewe ni wa pekee. Hakuna mtu ambaye atakuja kufanana na wewe. Fanya kitu ambacho ukikifanya kinaweza kuwafikia wengine.  Na kitu kizuri ambacho unaweza kukifanya na kuendelea ni kuandika. Unaweza kutengeneza blog na kuanza kuandika makala ambazo zitawafikia watu wengi au unaweza kuwa unaandika vitabu. Njia hii ya kuandika mara nyingi inawafikia watu wengi kuweza kupata maarifa ambayo yanaweza kudumu kwa muda mrefu.

3.           Kimwili: Mwili wako ndio mali kwako
Miili yetu ni thamani muhimu kwetu. Tumezaliwa tuweze kutumia maarifa yetu yote. Hakuna mtu wala jambo la kulaumu katika maisha yetu.  Miili yetu ina nguvu za kutosha kuweza kufanya kitu chochote. Tumia nguvu ulizonazo kwenye mwili wako katika kufanya mambo yaliyo bora yanayoweza kukufanya wewe uonekana shujaa wa maisha yako.

4.           Kiroho: Angalia Imani Yako
Jenga hisia ya kuiona dunia kama ina maana sana kwako. Sote tuna kitu ambacho huzifanya roho zetu zipate Amani na furaha.  Fanya unachofanya kwa uaminifu na kwa moyo wa upendo. Unapofanya kwa roho ya upendo na uaminifu unakuwa umetengeneza heshima ya kutambuliwa na kukumbukwa daima.

5.           Akili: Akili yako ndio kitovi cha udhibiti
Akili zetu ndizo zinazotuongoza nini tufanye. Mawazo yako yaweke katika kuwasaidia watu wengine kupata kile wanachokihitaji kwenye maisha yao. Thamini watu wote na ishi kwa kuwa na msaada kwa maisha ya watu wengine. Jitoe katika kuwafanya wengine wawe na maisha bora.

Hizi ndio njia tano bora za kuishi maisha yako ili watu waweze kukukumbuka. Chagua kuishi kwa kufuata njia hizi kwa ajili ya kuacha athari kwenye dunia hii.
 
Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja  kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

Jumamosi, 19 Novemba 2016

Zijue Mbinu Za Kuendeleza Mawazo Ya Mafaniko


 Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

Leo hii napenda kuendelea kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mbinu za kuendeleza mawazo ya mafanikio.

Kama ungependa kuwa na mafanikio Zaidi katika maisha yako, fanyia kazi mawazo yako ili uweze kupata muongozo wa mafanikio.

Na hizi hapa ndio mbinu ninazokushauru uziendeleze kwa ajili ya mafanikio yako.

1.           Jifunze Kutafakari kwa Mtazamo Mpana
Ondoa Dhana ya kwamba haiwezekani kwenye jambo lolote unalofanya. Unapoweza kufikiria mambo makubwa na kuamini kwamba inawezekana, hapo ndipo akili yako inapoweza kuwa na mtazamo wa kuweza kufanya bila kushindwa. Kila kitu kinawezekana, ni juu yako wewe dhidi ya kufanya kwa upendo na kwa bidii ili kuweza kufikia maisha ya mafanikio. Waza mambo makubwa ambayo yatakupeleka hatua kumi mbele kufika kwenye maisha ya mafanikio. Na unapoamua kufanya usikate tamaa.

2.           Fanya Maamuzi Sasa kwa Ajili Ya Kuweza Kuishi Maisha Mazuri Baadaye
Fikiria maisha yako ya usoni. Huwezi kufanikiwa kwenye maisha yako bila ya kuwa na mtazamo wa baadaye. Lazima uishi kwa kufanya mambo ya msingi sasa ili uweze kuishi vizuri baadaye. Lazima ufikirie ni maisha ya aina gani unataka kuishi.

Mtazamo wa baadaye unaweza kukuongoza katika kufanya maamuzi yako ya kuishi maisha ya kila siku.

3.           Chukua Hatua Kwenye Wakati Mgumu
Moja ya njia mzuri ya kujenga kujiamini ni kuchukua hatua kwenye hali isiyo ya kawaida. Unapoweza kujifunza kufanya kwenye wakati mgumu unakuwa umetengeneza uwezo wako wa kuwa jasiri na kuwa na kasi ya kujenga. Chukua hatua moja kila siku ya kufanya jambo ambalo hujatarajia kulifanya. Jifunze kufanya kitu hata kama unaogopa kufanya. Fanyia kazi malengo makubwa na jenga maisha yako kwa ndoto ambazo zitakutoa kwenye hali ya kawaida.
 
Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja  kwenye email yako.
Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
  0784498867 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

Jumanne, 15 Novemba 2016

Jifunze Njia Tatu (03) Za Kufikiria Kama Milionia


  Habari za leo ndugu msomaji wa nyota ya mtanzania. Ni siku nyengine tena tunakuletea mfululizo wa makala zetu za kila siku. Nina imani kwamba unapata maarifa ya kutosha.

 Leo hii napenda kuwashirikisha wasomaji wetu makala inayohusiana na mambo matatu ya kujifunza ili uweze kufikiria kama milionia.

Watu wengi wanadhani kwamba kuwa milionia ni suala la kuja na wazo la biashara au kufanya kazi kwenye makampuni makubwa. Wanashindwa kuelewa kwamba watu ambao wanamafanikio wanaishi kwa kutegemea kupata pesa kama kawaida.

Njia ya kuwa huru kifedha haitokani na kipato unachokipata bali ni ule uwezo wa kufanya na kufikiri kuhusu pesa.

Kwenye Makala hii nitakushirikisha  mambo matatu muhimu na mawazo sahihi kuhusiana na kuweza kuwa milionia. Kuweza kufanikisha mambo hayo sio tu  kwamba ni uhakika wa kuwa milionia, lakini ni njia za uhakika za kufanya maamuzi yalio sahihi.

1.           Jifunze Tofauti Kati Ya Mali Na Madeni
Nadhani ninapoongelea maana ya mali utakuwa unanielewa. Mali Inaweza kuwa vitu kama Nyumba, Uwekezaji na  Fedha zinazoweza kukuongezea thamani.

Chukulia mfano unataka kunua gari. Gari kwa kiasi Fulani inayo thamani lakini jiulize gari ulilonunua linakuingizia shilingi kwenye mifuko yako? Kama haiwezi kukuongezea pato lako basi hiyo hatuwezi kuita mali bali gari hilo tunaweza kusema ni deni kwako kwa sababu linapunguza pesa kwenye mifuko yako.

Kama gari hilo unalitumia kama daladala au taxi basi tunaweza kuliita ni mali kwa sababu linatengeneza pesa kila siku.

Unapoweza kufikiria kwa mtazamo huo utagundua kwamba matumizi ya pesa yako yanatakiwa yatumike pale ambapo pesa inaweza kuzalisha.

2.           Tambua Njia Za Kuzalisha Mapato
Watu wengi wanapatia maisha kutokana na kufanya kazi. Kufanya kazi ni njia ya uhakika ya kuzalisha kipato. Ni lazima ufanye kazi kila siku kama unataka kuzalisha kipato. Unaposimama kufanya kazi basi utakuwa umesimama kutengeneza pesa.

Utajiri wako unategemea ni kiasi gani unajituma kufanya kazi.

Kwa watu wengi kuzalisha mapato ni suala rahisi la kufanya ambalo hufanywa kwa kuwekeza pesa. Kuwekeza kwenye hisa ni uwekezaji mzuri kwa sababu hauhitaji uwepo wako wa moja kwa moja. Milionia wengi wanakuwa na vyanzo mbali mbali vya kuongeza kipato.

Kumbuka uwekezaji sio lazima uwekeze pesa. Bali pia unaweza kuwekeza muda. Kutengeneza biashara ambayo ina uwezo wa kujiendesha wenyewe, kama tovuti, ambayo inahitaji kazi kidogo. Kazi inapokamilika inakuwa inaendelea kwa kutumia mfumo ambao unajiendesha wenyewe.

3.           Ishi Chini Ya Njia Yako.
Haijalishi kwamba unatengeneza kiasi cha milioni mia moja kwa mwaka au milioni moja kwa mwaka, jambo la muhimu ni kwamba unaishi maishi ya kawaida. Usiwe kama wale watu ambao wanatumia tabia ya asili ya kuwa na matumizi makubwa pale ambapo wanapata pesa nyingi. Kumbuka kujenga tabia ya kutunza pesa Zaidi unavyoweza. Hata kama unapata laki moja kwa mwezi , unaweza kuanza.

Wakati mwengine mapato yako yanaweza kuongezeka, na hiyo ndiyo iwe njia ya kuongeza uwekezaji wako. Jaribu kuongeza fedha inayoongezeka kwenye akiba yako, badala ya matumizi hakikisha unaboresha maisha yako.

Hakikisha unajifunza na kufuata njia hizi zitakazo kuvuusha kufikia milionia. Jifunze tofauti kati ya mali na madeni, Tambua njia za kuzalisha mapato na Ishi chni ya njia yako. 
 
Weka email yako hapa na bonyeza NIUNGE ili kuweza kupokea Makala moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu Kwenye Blog Yako Uipendayo.
Wako Wa Karibu,
Ali Khamis.
Tuwasiliane Kupitia
0784498867
 

Jiunge Kupata Makala hizi

* indicates required


Share:

JIUNGE NA NYOTA YA MTANZANIA

* indicates required

CHAGUA MWEZI WA MAKALA